< Luc 4 >

1 Jésus, rempli du Saint-Esprit, revint du Jourdain, et fut conduit par l'Esprit dans le désert,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 Où il fut tenté par le diable pendant quarante jours, et il ne mangea rien durant ces jours-là; mais après qu'ils furent passés, il eut faim.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Alors le diable lui dit: Si tu es le Fils de Dieu, commande à cette pierre qu'elle devienne du pain.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Et Jésus lui répondit: Il est écrit: L'homme ne vivra pas seulement de pain, mais de toute parole de Dieu.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Ensuite le diable le mena sur une haute montagne, et lui fit voir en un moment tous les royaumes du monde;
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 Et le diable lui dit: Je te donnerai toute cette puissance et la gloire de ces royaumes; car elle m'a été donnée, et je la donne à qui je veux.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Si donc tu te prosternes devant moi, toutes choses seront à toi.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Mais Jésus lui répondit: Arrière de moi, Satan; car il est écrit: Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu le serviras lui seul.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 Il le mena aussi à Jérusalem, et il le mit sur le haut du temple, et lui dit: Si tu es le Fils de Dieu, jette-toi d'ici en bas;
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 Car il est écrit, qu'il ordonnera à ses anges d'avoir soin de toi, pour te garder;
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 Et qu'ils te porteront dans leurs mains, de peur que ton pied ne heurte contre quelque pierre.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Mais Jésus lui répondit: Il est dit: Tu ne tenteras pas le Seigneur ton Dieu.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Et le diable ayant achevé toute la tentation, se retira de lui pour un temps.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Et Jésus s'en retourna en Galilée, par le mouvement de l'Esprit, et sa réputation courut par tout le pays d'alentour.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Car il enseignait dans leurs synagogues, et il était honoré de tout le monde.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Et Jésus vint à Nazareth, où il avait été élevé, et il entra, selon sa coutume, le jour du sabbat, dans la synagogue, et il se leva pour lire.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 Et on lui présenta le livre du prophète Ésaïe, et ayant déroulé le livre, il trouva l'endroit où il était écrit:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 L'Esprit du Seigneur est sur moi, c'est pourquoi il m'a oint pour annoncer l'Évangile aux pauvres; il m'a envoyé pour guérir ceux qui ont le cœur brisé;
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 Pour publier la liberté aux captifs, et le recouvrement de la vue aux aveugles; pour renvoyer libres ceux qui sont dans l'oppression, et pour publier l'année favorable du Seigneur.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Et ayant replié le livre, et l'ayant rendu au ministre, il s'assit; et les yeux de tous, dans la synagogue, étaient arrêtés sur lui.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Alors il commença à leur dire: Cette parole de l'Écriture est accomplie aujourd'hui, et vous l'entendez.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Tous lui rendaient témoignage, et admiraient les paroles de grâce qui sortaient de sa bouche, et ils disaient: N'est-ce pas le fils de Joseph?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Et il leur dit: Vous me direz sans doute ce proverbe: Médecin, guéris-toi toi-même; fais aussi ici, dans ta patrie, tout ce que nous avons entendu dire que tu as fait à Capernaüm.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Mais il dit: Je vous dis en vérité que nul prophète n'est reçu dans sa patrie.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 Je vous dis en vérité: Il y avait plusieurs veuves en Israël au temps d'Élie, lorsque le ciel fut fermé trois ans et six mois, tellement qu'il y eut une grande famine par tout le pays.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 Néanmoins Élie ne fut envoyé chez aucune d'elles; si ce n'est chez une femme veuve de Sarepta, en Sidon.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Il y avait aussi plusieurs lépreux en Israël au temps d'Élisée le prophète; toutefois aucun d'eux ne fut guéri; si ce n'est Naaman, le Syrien.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Et ils furent tous remplis de colère, dans la synagogue, en entendant ces choses.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Et s'étant levés ils le chassèrent de la ville, et le menèrent jusqu'au sommet escarpé de la montagne sur laquelle leur ville était bâtie, pour le précipiter.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Mais lui, passant au milieu d'eux, s'en alla.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Et il descendit chez les gens de Capernaüm, ville de Galilée, et il les enseignait les jours de sabbat.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 Et ils étaient étonnés de sa doctrine; car il parlait avec autorité.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Or, il y avait dans la synagogue un homme possédé d'un esprit immonde, qui s'écria à voix haute:
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 Ah! qu'y a-t-il entre nous et toi, Jésus de Nazareth? Es-tu venu pour nous perdre? Je sais qui tu es: le Saint de Dieu.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Et Jésus, le menaçant, lui dit: Tais-toi, et sors de cet homme. Et le démon, après l'avoir renversé au milieu de l'assemblée, sortit de lui, sans lui faire aucun mal.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Et ils en furent tous épouvantés, et ils disaient entre eux: Qu'est-ce que ceci? Il commande avec autorité et avec puissance aux esprits immondes, et ils sortent!
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 Et sa réputation se répandit dans tous les quartiers du pays d'alentour.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Jésus, étant sorti de la synagogue, entra dans la maison de Simon. Or, la belle-mère de Simon avait une fièvre violente; et ils le prièrent en sa faveur.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 S'étant donc penché sur elle, il commanda à la fièvre, et la fièvre la quitta; et aussitôt elle se leva et les servit.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Quand le soleil fut couché, tous ceux qui avaient des malades atteints de diverses maladies, les lui amenèrent; et il les guérit en imposant les mains à chacun d'eux.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Les démons sortaient aussi de plusieurs, criant et disant: Tu es le Christ, le Fils de Dieu; mais il les censurait, et ne leur permettait pas de dire qu'ils sussent qu'il était le Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Et dès que le jour parut, il sortit et alla dans un lieu désert, et une multitude de gens qui le cherchaient, vinrent jusqu'à lui et ils voulaient le retenir, afin qu'il ne les quittât pas.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Mais il leur dit: Il faut que j'annonce aussi le royaume de Dieu aux autres villes; car c'est pour cela que j'ai été envoyé.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Et il prêchait dans les synagogues de la Galilée.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luc 4 >