< Marc 2 >

1 Quelque temps après, [Jésus] revint à Capharnaüm. Lorsqu’on entendit qu’il était dans la maison,
Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
2 il s’y assembla aussitôt un si grand nombre [de personnes], qu’elles ne pouvaient trouver place, pas même aux abords de la porte; et il leur annonçait la parole.
Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
3 Alors on lui amena un paralytique porté par quatre [hommes].
Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
4 Et, comme ils ne pouvaient le lui présenter à cause de la foule, ils découvrirent le toit à l’endroit où il était, et par l’ouverture ils descendirent le grabat où gisait le paralytique.
Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
5 Jésus, voyant leur foi, dit au paralytique: « [Mon] fils, tes péchés te sont remis. »
Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 Or il y avait là quelques scribes assis, qui pensaient dans leur cœur:
Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
7 « Comment cet homme parle-t-il ainsi? Il blasphème. Qui peut remettre les péchés sinon Dieu seul? »
“Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
8 Jésus, ayant aussitôt connu par son esprit qu’ils pensaient ainsi en eux-mêmes, leur dit: « Pourquoi avez-vous de telles pensées dans vos cœurs?
Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
9 Lequel est le plus facile de dire au paralytique: Tes péchés te sont remis, ou [de lui] dire: Lève-toi, prends ton grabat et marche?
Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
10 Mais afin que vous sachiez que le Fils de l’homme a sur la terre, le pouvoir de remettre les péchés, – [Jésus] s’adressa au paralytique –
Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
11 je te le commande: Lève-toi, prends ton grabat et va dans ta maison. »
“Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
12 Et à l’instant celui-ci se leva, prit son grabat, et sortit en présence de tous, de sorte que tout le peuple était dans l’admiration et rendait gloire à Dieu, en disant: « Jamais nous n’avons rien vu de semblable. »
Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
13 Jésus sortit de nouveau le long de la mer; et toute la foule venait à lui, et il les enseignait.
Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
14 En passant, il vit Lévi, fils d’Alphée, assis au bureau de péage; il lui dit: « Suis-moi. » Lévi se leva et le suivit.
Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
15 Il arriva que Jésus étant à table dans la maison de cet homme, plusieurs publicains et gens de mauvaise vie se trouvaient à table avec lui et ses disciples, car ils étaient nombreux à le suivre.
Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
16 Les scribes et les Pharisiens, le voyant manger avec des pécheurs et des publicains, disaient à ses disciples: « D’où vient que votre Maître mange et boit avec des pécheurs et des publicains? »
Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
17 Entendant cela, Jésus leur dit: « Ce ne sont pas ceux qui se portent bien qui ont besoin de médecin, mais les malades; je ne suis pas venu appeler les justes, mais les pécheurs. »
Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
18 Les disciples de Jean et les Pharisiens avaient coutume de jeûner. Ils vinrent le trouver et lui dirent: « Pourquoi, tandis que les disciples de Jean et ceux des Pharisiens pratiquent le jeûne, vos disciples ne jeûnent-ils pas? »
Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
19 Jésus leur répondit: « Les compagnons de l’époux peuvent-ils jeûner pendant que l’époux est avec eux? Aussi longtemps qu’ils ont avec eux l’époux, ils ne peuvent pas jeûner.
Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
20 Mais les jours viendront où l’époux leur sera enlevé, et alors ils jeûneront en ces jours-là.
Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
21 Personne ne coud une pièce d’étoffe neuve à un vieux vêtement: autrement la pièce neuve emporte un morceau du vieux, et la déchirure devient pire.
Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
22 Et personne ne met du vin nouveau dans des outres vieilles: autrement, le vin fait rompre les outres et le vin se répand, et les outres sont perdues. Mais le vin nouveau doit se mettre dans des outres neuves. »
Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
23 Il arriva, un jour de sabbat, que Jésus traversait des champs de blé, et ses disciples, tout en s’avançant, se mirent à cueillir des épis.
Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
24 Les Pharisiens lui dirent: « Voyez donc! Pourquoi font-ils, le jour du sabbat, ce qui n’est pas permis? »
Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
25 Il leur répondit: « N’avez-vous jamais lu ce que fit David lorsqu’il fut dans le besoin, ayant faim, lui et ceux qui l’accompagnaient:
Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
26 comment il entra dans la maison de Dieu, au temps du grand prêtre Abiathar, et mangea les pains de proposition, qu’il n’est permis de manger qu’aux prêtres seuls, et en donna même à ceux qui étaient avec lui? »
Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
27 Il leur dit encore: « Le sabbat a été fait pour l’homme, et non l’homme pour le sabbat;
Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
28 c’est pourquoi le Fils de l’homme est maître même du sabbat. »
Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”

< Marc 2 >