< Matthew 4 >

1 Thanne Jhesus was led of a spirit in to desert, to be temptid of the feend.
Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
2 And whanne he hadde fastid fourti daies and fourti nyytis, aftirward he hungride.
Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
3 And the tempter cam nyy, and seide to hym, If thou art Goddis sone, seie that thes stoones be maad looues.
Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
4 Which answeride, and seide to hym, It is writun, Not oonli in breed luyeth man, but in ech word that cometh of Goddis mouth.
Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
5 Thanne the feend took hym in to the hooli citee, and settide hym on the pynacle of the temple,
Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
6 and seide to hym, If thou art Goddis sone, sende thee adoun; for it is writun, That to hise aungels he comaundide of thee, and thei schulen take thee in hondis, lest perauenture thou hirte thi foot at a stoon.
akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
7 Eftsoone Jhesus seide to hym, It is writun, Thou shalt not tempte thi Lord God.
Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
8 Eftsoone the feend took hym in to a ful hiy hil, and schewide to hym alle the rewmes of the world, and the ioye of hem;
Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
9 and seide to hym, Alle these `Y schal yyue to thee, if thou falle doun and worschipe me.
kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
10 Thanne Jhesus seide to hym, Goo, Sathanas; for it is writun, Thou schalt worschipe thi Lord God, and to hym aloone thou shalt serue.
Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
11 Thanne the feend lafte hym; and lo! aungels camen nyy, and serueden to hym.
Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
12 But whanne Jhesus hadde herd that Joon was takun, he wente in to Galilee.
Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
13 And he lefte the citee of Nazareth, and cam, and dwelte in the citee of Cafarnaum, biside the see, in the coostis of Zabulon and Neptalym,
Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
14 that it shulde be fulfillid, that was seid by Ysaie, the profete, seiynge,
ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
15 The lond of Sabulon and the lond of Neptalym, the weie of the see ouer Jordan, of Galilee of hethen men,
“Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
16 the puple that walkide in derknessis saye greet liyt, and while men satten in the cuntre of shadewe of deth, liyt aroos to hem.
watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
17 Fro that tyme Jhesus bigan to preche, and seie, Do ye penaunce, for the kyngdom of heuenes schal come niy.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
18 And Jhesus walkide bisidis the see of Galilee, and saye twei britheren, Symount, that is clepid Petre, and Andrewe, his brothir, castynge nettis in to the see; for thei weren fischeris.
Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
19 And he seide to hem, Come ye aftir me, and Y shal make you to be maad fisscheris of men.
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
20 And anoon thei leften the nettis, and sueden hym.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21 And he yede forth fro that place, and saie tweyne othere britheren, James of Zebede, and Joon, his brother, in a schip with Zebede, her fadir, amendynge her nettis, and he clepide hem.
Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
22 And anoon thei leften the nettis and the fadir, and sueden hym.
Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
23 And Jhesus yede aboute al Galilee, techynge in the synagogis of hem, and prechynge the gospel of the kyngdom, and heelynge euery languor and eche sekenesse among the puple.
Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
24 And his fame wente in to al Sirie; and thei brouyten to hym alle that weren at male ese, and that weren take with dyuerse languores and turmentis, and hem that hadden feendis, and lunatike men, and men in palesy, and he heelide hem.
Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
25 And ther sueden hym myche puple of Galile, and of Decapoli, and of Jerusalem, and of Judee, and of biyende Jordan.
Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.

< Matthew 4 >