< Acts 4 >

1 And while thei spaken to the puple, the preestis and magistratis of the temple, and the Saduceis camen vpon hem, and soreweden,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
2 that thei tauyten the puple, and telden in Jhesu the ayenrisyng fro deth.
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
3 And thei leiden hondis on hem, and puttiden hem in to warde in to the morewe; for it was thanne euentid.
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
4 But manye of hem that hadden herd the word, bileueden; and the noumbre of men was maad fyue thousyndis.
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
5 And amorewe it was don, that the princis of hem, and eldre men and scribis weren gadirid in Jerusalem;
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
6 and Annas, prince of preestis, and Caifas, and Joon, and Alisaundre, and hou manye euere weren of the kynde of preestis.
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
7 And thei settiden hem in the myddil, and axiden, In what vertue, ether in what name, han ye don this thing?
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
8 Thanne Petre was fillid with the Hooli Goost, and seide to hem, Ye pryncis of the puple, and ye eldre men, here ye.
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
9 If we to dai be demyd in the good dede of a sijk man, in whom this man is maad saaf,
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
10 be it knowun to you alle, and to al the puple of Israel, that in the name of Jhesu Crist of Nazareth, whom ye crucifieden, whom God reiside fro deth, in this this man stondith hool bifor you.
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
11 This is the stoon, which was repreued of you bildinge, which is maad in to the heed of the corner;
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 and heelthe is not in ony othir. For nether other name vndur heuene is youun to men, in which it bihoueth vs to be maad saaf.
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
13 And thei siyen the stidfastnesse of Petre and of Joon, for it was foundun that thei weren men vnlettrid, and lewid men, and thei wondriden, and knewen hem that thei weren with Jhesu.
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
14 And thei siyen the man that was helid, stondinge with hem, and thei myyten no thing ayenseie.
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
15 But thei comaundiden hem to go forth with out the counsel. And thei spaken togidere,
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
16 and seiden, What schulen we do to these men? for the signe is maad knowun bi hem to alle men, that dwellen at Jerusalem; it is opyn, and we moun not denye.
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
17 But that it be no more pupplischid in to the puple, manasse we to hem, that thei speke no more in this name to ony men.
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
18 And thei clepiden hem, and denounsiden to hem, that on no maner thei schulden speke, nether teche, in the name of Jhesu.
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 But Petre and Joon answeriden, and seiden to hem, If it be riytful in the siyt of God to here you rather than God, deme ye.
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
20 For we moten nedis speke tho thingis, that we han sayn and herd.
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
21 And thei manassiden, and leften hem, and foundun not hou thei schulden punische hem, for the puple; for alle men clarifieden that thing that was don in that that was bifalle.
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
22 For the man was more than of fourty yeer, in which this signe of heelthe was maad.
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
23 And whanne thei weren delyuerid, thei camen to her felowis, and telden to hem, hou grete thingis the princis of preestis and the eldre men hadden seid to hem.
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
24 And whanne thei herden, with oon herte thei reiseden vois to the Lord, and seiden, Lord, thou that madist heuene and erthe, see, and alle thingis that ben in hem, which seidist bi the Hooli Goost,
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
25 bi the mouth of oure fadir Dauid, thi child, Whi hethen men gnastiden with teeth togidre, and the puplis thouyten veyn thingis?
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
26 Kyngis of the erthe stoden nyy, and princis camen togidre `in to oon, ayens the Lord, and ayens his Crist.
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
27 For verili Eroude and Pounce Pilat, with hethene men, and puplis of Israel, camen togidre in this citee ayens thin hooli child Jhesu,
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
28 whom thou anoyntidist, to do the thingis, that thin hoond and thi counsel demyden to be don.
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
29 And now, Lord, biholde in to the thretnyngis of hem, and graunte to thi seruauntis to speke thi word with al trist,
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
30 in that thing that thou holde forth thin hond, that heelthis and signes and wondris be maad bi the name of thin hooli sone Jhesu.
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
31 And whanne thei hadden preyed, the place was moued, in which thei weren gaderid; and alle weren fillid with the Hooli Goost, and spaken the word of God with trist.
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
32 And of al the multitude of men bileuynge was oon herte and oon wille; nether ony man seide ony thingis of tho thingis that he weldide to be his owne, but alle thingis weren comyn to hem.
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
33 And with greet vertu the apostlis yeldiden witnessyng of the ayenrysyng of Jhesu Crist oure Lord, and greet grace was in alle hem.
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
34 For nether ony nedi man was among hem, for how manye euere weren possessouris of feeldis, ether of housis, thei seelden, and brouyten the pricis of tho thingis that thei seelden,
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
35 and leiden bifor the feet of the apostlis. And it was departid to ech, as it was nede to ech.
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
36 Forsothe Joseph, that was named Barsabas of apostlis, that is to seie, the sone of coumfort, of the lynage of Leuy,
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
37 a man of Cipre, whanne he hadde a feeld, seelde it, and brouyte the prijs, and leide it bifor the feet of apostlis.
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< Acts 4 >