< 2 Timothy 4 >

1 I witnesse bifore God and Crist Jhesu, that schal deme the quike and the deed, and bi the comyng of hym, and the kyngdom of hym,
Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2 preche the word, be thou bisi couenabli with outen rest, repreue thou, biseche thou, blame thou in al pacience and doctryn.
hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3 For tyme schal be, whanne men schulen not suffre hoolsum teching, but at her desiris thei schulen gadere `togidere to hem silf maistris yitchinge to the eeris.
Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4 And treuli thei schulen turne awei the heryng fro treuthe, but to fablis thei schulen turne.
Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5 But wake thou, in alle thingis traueile thou, do the werk of an euangelist, fulfille thi seruyce, be thou sobre.
Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6 For Y am sacrifisid now, and the tyme of my departyng is nyy.
Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7 Y haue stryuun a good strijf, Y haue endid the cours, Y haue kept the feith.
Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8 In `the tothir tyme a coroun of riytwisnesse is kept to me, which the Lord, a iust domesman, schal yelde to me in that dai; and not oneli to me, but also to these that louen his comyng.
Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9 Hyye thou to come to me soone.
Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10 For Demas, louynge this world, hath forsakun me, and wente to Tessalonyk, Crescens in to Galathi, Tite in to Dalmacie; (aiōn g165)
Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn g165)
11 Luk aloone is with me. Take thou Mark, and brynge with thee; for he is profitable to me in to seruyce.
Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12 Forsothe Y sente Titicus to Effesi.
Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13 The cloth which Y lefte at Troade at Carpe, whanne thou comest, bringe with thee, and the bookis, but moost parchemyne.
Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14 Alisaundre, the tresorer, schewide to me myche yuele; `the Lord schal yelde to hym aftir his werkis.
Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15 Whom also thou eschewe; for he ayenstood ful greetli oure wordis.
Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16 In my firste defence no man helpide me, but alle forsoken me; be it not arettid to hem.
Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17 But the Lord helpide me, and coumfortide me, that the preching be fillid bi me, and that alle folkis here, that Y am delyueride fro the mouth of the lioun.
Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18 And the Lord delyueride me fro al yuel werk, and schal make me saaf in to his heuenly kingdom, to whom be glorie in to worldis of worldis. (aiōn g165)
Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
19 Amen. Grete wel Prisca, and Aquila, and the hous of Oneseforus.
Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20 Erastus lefte at Corynthi, and Y lefte Trofymus sijk at Mylete.
Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21 Hiye thou to come bifore wyntir. Eubolus, and Prudent, and Lynus, and Claudia, and alle britheren, greten thee wel.
Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22 Oure Lord Jhesu Crist be with thi spirit. The grace of God be with you. Amen.
Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.

< 2 Timothy 4 >