< 2 Timothy 4 >

1 I witnesse bifore God and Crist Jhesu, that schal deme the quike and the deed, and bi the comyng of hym, and the kyngdom of hym,
Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
2 preche the word, be thou bisi couenabli with outen rest, repreue thou, biseche thou, blame thou in al pacience and doctryn.
Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
3 For tyme schal be, whanne men schulen not suffre hoolsum teching, but at her desiris thei schulen gadere `togidere to hem silf maistris yitchinge to the eeris.
Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
4 And treuli thei schulen turne awei the heryng fro treuthe, but to fablis thei schulen turne.
Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
5 But wake thou, in alle thingis traueile thou, do the werk of an euangelist, fulfille thi seruyce, be thou sobre.
Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
6 For Y am sacrifisid now, and the tyme of my departyng is nyy.
Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
7 Y haue stryuun a good strijf, Y haue endid the cours, Y haue kept the feith.
Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
8 In `the tothir tyme a coroun of riytwisnesse is kept to me, which the Lord, a iust domesman, schal yelde to me in that dai; and not oneli to me, but also to these that louen his comyng.
Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
9 Hyye thou to come to me soone.
Jitahidi kuja kwagu haraka.
10 For Demas, louynge this world, hath forsakun me, and wente to Tessalonyk, Crescens in to Galathi, Tite in to Dalmacie; (aiōn g165)
Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn g165)
11 Luk aloone is with me. Take thou Mark, and brynge with thee; for he is profitable to me in to seruyce.
Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
12 Forsothe Y sente Titicus to Effesi.
Nimemtuma Tikiko Efeso.
13 The cloth which Y lefte at Troade at Carpe, whanne thou comest, bringe with thee, and the bookis, but moost parchemyne.
Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
14 Alisaundre, the tresorer, schewide to me myche yuele; `the Lord schal yelde to hym aftir his werkis.
Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
15 Whom also thou eschewe; for he ayenstood ful greetli oure wordis.
Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
16 In my firste defence no man helpide me, but alle forsoken me; be it not arettid to hem.
Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
17 But the Lord helpide me, and coumfortide me, that the preching be fillid bi me, and that alle folkis here, that Y am delyueride fro the mouth of the lioun.
Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
18 And the Lord delyueride me fro al yuel werk, and schal make me saaf in to his heuenly kingdom, to whom be glorie in to worldis of worldis. (aiōn g165)
Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn g165)
19 Amen. Grete wel Prisca, and Aquila, and the hous of Oneseforus.
Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
20 Erastus lefte at Corynthi, and Y lefte Trofymus sijk at Mylete.
Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
21 Hiye thou to come bifore wyntir. Eubolus, and Prudent, and Lynus, and Claudia, and alle britheren, greten thee wel.
Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
22 Oure Lord Jhesu Crist be with thi spirit. The grace of God be with you. Amen.
Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.

< 2 Timothy 4 >