< Mark 2 >

1 And after some days He went again into Capernaum; and it being heard that He was in the house,
Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
2 great numbers were immediately gathered together, so that there was no more room to contain them, not even about the door: and as he was preaching the word unto them,
Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
3 there came some to Him, bringing a paralytic who was carried by four men:
Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
4 and not being able to come near to Him for the croud, they uncovered the roof where He was, and when they had made an openning, they let down the couch on which the paralytic was laid.
Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
5 And Jesus, seeing their faith, saith to him that had the palsy, Son, thy sins are forgiven thee.
Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 But there were some of the scribes sitting there, and reasoning in their hearts,
Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
7 Why doth this man thus speak blasphemies? who can forgive sins but God?
“Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
8 And Jesus, who knew immediately in his spirit that they were thus reasoning within themselves, said unto them, Why do ye dispute these things in your hearts?
Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
9 Which is easier, to say to the paralytic, Thy sins are forgiven; or to say, Rise, take up thy couch, and walk?
Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
10 But that ye may know, that the Son of man hath power on earth to forgive sins,
Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
11 I say unto thee (saith He to the paralytic, ) Arise, and take up thy couch, and go thy way to thine own house.
“Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
12 And he instantly arose, and taking up his couch, went out before them all, so that they were all amazed, and glorified God, saying, we never saw the like.
Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
13 And He went out again towards the sea-side, and all the people resorted to Him, and He taught them.
Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
14 And as He went along, He saw Levi the son of Alpheus, sitting at the receit of custom, and saith unto him, Follow me: and he rose up and followed Him.
Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
15 And as He sat at table in his house, many publicans and sinners also sat down with Jesus and his disciples: for there were many, and they followed Him.
Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
16 And the scribes and pharisees, when they saw Him eating with publicans and sinners, said to his disciples, What is the meaning that He eateth with publicans and sinners?
Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
17 Which Jesus hearing, saith unto them, They that are in health have no need of a physician, but they that are ill: I came not to call the righteous, but sinners.
Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
18 And as the disciples of John, and of the pharisees used to fast, they came to Him, saying, Why do the disciples of John and of the pharisees fast, but thy disciples fast not?
Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
19 And Jesus said unto them, Can the bridemen fast, when the bridegroom is with them? while the bridegroom is with them, they cannot fast:
Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
20 but the days will come, when the bridegroom shall be taken from them; and then shall they fast.
Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
21 No man seweth a piece of new cloth on an old garment; otherwise, it's new patch teareth from the old, and the rent is made worse:
Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
22 nor does any one put new wine into old vessels; otherwise the new wine bursteth the vessels, and the wine is spilt, and the vessels are destroyed: but new wine should be put into new vessels.
Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
23 And as He was going thro' the corn-fields on the sabbath-day, his disciples began as they went along to pluck the ears of corn.
Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
24 And the pharisees said to Him, See, why do they what is not lawful to be done on the sabbath-day?
Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
25 And He said unto them, Have ye never read what David did, in his necessity, when he was hungry, himself and those that were with him?
Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
26 how he went into the house of God in the days of Abiathar, who was afterwards the high priest, and did eat the shew-bread, which it is not lawful for any to eat, but the priests, and gave also to them that were with him!
Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
27 And He said moreover unto them, The sabbath was made for man, not man for the sabbath:
Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
28 and therefore the Son of man is Lord even of the sabbath.
Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”

< Mark 2 >