< 1 Samuel 8 >

1 When Samuel was old, he made his sons judges over Israel.
Samweli alipozeeka, aliwaweka watoto wake wawe waamuzi juu ya Israeli.
2 Now the name of his firstborn was Joel, and the name of his second, Abijah. They were judges in Beersheba.
Mtoto wake wa kwanza aliitwa Yoeli, na mtoto wake wa pili aliitwa Abiya. Hawa walikuwa waamuzi katika Bersheba.
3 His sons didn’t walk in his ways, but turned away after dishonest gain, took bribes, and perverted justice.
Watoto wake hawakuenenda katika njia za baba yao, bali walipiga mbio kutafuta mapato ya udhalimu. Walipokea rushwa na na kupotosha hukumu.
4 Then all the elders of Israel gathered themselves together and came to Samuel to Ramah.
Ndipo wazee wote wa Israeli walikutana pamoja na kumwendea Samweli huko Rama.
5 They said to him, “Behold, you are old, and your sons don’t walk in your ways. Now make us a king to judge us like all the nations.”
Wakamwambia, “Angalia, wewe umekuwa mzee, na watoto wako hawaenendi katika njia zako. Tuchagulie mfalme wakutuamua kama yalivyo mataifa yote.”
6 But the thing displeased Samuel when they said, “Give us a king to judge us.” Samuel prayed to the LORD.
Lakini haikumpendeza Sameli waliposema, “Utupatie mfalme wa kutuamua.” Hivyo akamwomba BWANA.
7 The LORD said to Samuel, “Listen to the voice of the people in all that they tell you; for they have not rejected you, but they have rejected me as the king over them.
Na BWANA akamwambia Samweli, “Sikiliza sauti ya watu kwa kila jambo wanalokwambia; kwa sababu hwajakukataa wewe, bali wamenikataa mimi nisiwe mfalme wao.
8 According to all the works which they have done since the day that I brought them up out of Egypt even to this day, in that they have forsaken me and served other gods, so they also do to you.
Sasa wanafanya kama vile walivyotenda tangu siku ile nilipowatoa huko Misri, kwa kuniacha, na kuwatumikia miungu mingine, na ndivyo hivyo pia wanakufanyia na wewe.
9 Now therefore, listen to their voice. However, you shall protest solemnly to them, and shall show them the way of the king who will reign over them.”
Basi sasa uwasikilize; lakini uwaonye sawasawa na uwafahamishe tabia ya mfalme atakaye waongoza.
10 Samuel told all the LORD’s words to the people who asked him for a king.
Kwa hiyo Samweli akawaambia watu waliokuwa wakiomba mfalme maneno yote ya BWANA.
11 He said, “This will be the way of the king who shall reign over you: he will take your sons and appoint them as his servants, for his chariots and to be his horsemen; and they will run before his chariots.
Akasema, “Hivi ndivyo jinsi mfalme atakavyowatawala.
12 He will appoint them to him for captains of thousands and captains of fifties; and he will assign some to plough his ground and to reap his harvest; and to make his instruments of war and the instruments of his chariots.
Atawachukua watoto wenu wa kiume na kuwaweka juu ya magari ya vita na kuwa wapanda farasi wake, na kukimbia mbele ya magari yake. Atawaweka ma- kapteni wake juu ya maelfu ya askari, na ma-kapteni juu ya askari hamsini. Wengine atawafanya wakulima wamashamba yake, wengine wavunaji wa mazao yake, wengine watatengeneza silaha zake na zana za magari yake.
13 He will take your daughters to be perfumers, to be cooks, and to be bakers.
Naye atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi, na waoka mikate.
14 He will take your fields, your vineyards, and your olive groves, even your best, and give them to his servants.
Atachukua mashamba yenu mazuri, mashamba ya mizabibu, na yale ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
15 He will take one tenth of your seed and of your vineyards, and give it to his officers and to his servants.
Atachukua moja ya kumi ya nafaka zenu na mizabibu na na kuwapa maofisa na watumishi wake.
16 He will take your male servants, your female servants, your best young men, and your donkeys, and assign them to his own work.
Atawachukua watumwa wenu na wajakazi wenu na vijana wenu waliowazuri na punda wenu; atawatumikisha wote kwa ajili yake.
17 He will take one tenth of your flocks; and you will be his servants.
Atawatoza moja ya kumi ya mifugo yenu, na mtakuwa watumwa wake.
18 You will cry out in that day because of your king whom you will have chosen for yourselves; and the LORD will not answer you in that day.”
Ndipo mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyemchagua kwa ajili yenu; lakini siku ile BWANA hatawajibu
19 But the people refused to listen to the voice of Samuel; and they said, “No, but we will have a king over us,
Lakini watu walikataa kumsikiliza Samweli; wakasema, “Hapana!” Lazima awepo mfalme juu yetu.
20 that we also may be like all the nations; and that our king may judge us, and go out before us, and fight our battles.”
Ili tuweze kuwa kama mataifa mengine yote, na hivyo mfalme wetu aweze kutuamua na atoke mbele yetu na atupiganie vita yetu.
21 Samuel heard all the words of the people, and he rehearsed them in the ears of the LORD.
Naye Samweli aliposikia maneno yote ya watu, akayarudia katika masiko ya BWANA.
22 The LORD said to Samuel, “Listen to their voice, and make them a king.” Samuel said to the men of Israel, “Everyone go to your own city.”
BWANA akamwambia Samweli, “Sikiliza sauti yao na uwafanyie mfalme.” Hivyo Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mtu na arudi mjini kwake.”

< 1 Samuel 8 >