< Ruth 4 >

1 Now Boaz went up to the gate and sat down there. Behold, the near kinsman of whom Boaz spoke came by. Boaz said to him, “Come over here, friend, and sit down!” He came over, and sat down.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 Boaz took ten men of the elders of the city, and said, “Sit down here,” and they sat down.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 He said to the near kinsman, “Naomi, who has come back out of the country of Moab, is selling the parcel of land, which was our brother Elimelech’s.
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 I thought I should tell you, saying, ‘Buy it before those who sit here, and before the elders of my people.’ If you will redeem it, redeem it; but if you will not redeem it, then tell me, that I may know. For there is no one to redeem it besides you; and I am after you.” He said, “I will redeem it.”
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 Then Boaz said, “On the day you buy the field from the hand of Naomi, you must buy it also from Ruth the Moabitess, the wife of the dead, to raise up the name of the dead on his inheritance.”
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 The near kinsman said, “I can’t redeem it for myself, lest I endanger my own inheritance. Take my right of redemption for yourself; for I can’t redeem it.”
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 Now this was the custom in former time in Israel concerning redeeming and concerning exchanging, to confirm all things: a man took off his sandal, and gave it to his neighbor; and this was the way of formalizing transactions in Israel.
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 So the near kinsman said to Boaz, “Buy it for yourself,” then he took off his sandal.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 Boaz said to the elders and to all the people, “You are witnesses today, that I have bought all that was Elimelech’s, and all that was Chilion’s and Mahlon’s, from the hand of Naomi.
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 Moreover, Ruth the Moabitess, the wife of Mahlon, I have purchased to be my wife, to raise up the name of the dead on his inheritance, that the name of the dead may not be cut off from among his brothers and from the gate of his place. You are witnesses today.”
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 All the people who were in the gate, and the elders, said, “We are witnesses. May Yahweh make the woman who has come into your house like Rachel and like Leah, which both built the house of Israel; and treat you worthily in Ephrathah, and be famous in Bethlehem.
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 Let your house be like the house of Perez, whom Tamar bore to Judah, of the offspring which Yahweh will give you by this young woman.”
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 So Boaz took Ruth and she became his wife; and he went in to her, and Yahweh enabled her to conceive, and she bore a son.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 The women said to Naomi, “Blessed be Yahweh, who has not left you today without a near kinsman. Let his name be famous in Israel.
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 He shall be to you a restorer of life and sustain you in your old age; for your daughter-in-law, who loves you, who is better to you than seven sons, has given birth to him.”
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 Naomi took the child, laid him in her bosom, and became nurse to him.
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 The women, her neighbors, gave him a name, saying, “A son is born to Naomi”. They named him Obed. He is the father of Jesse, the father of David.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 Now this is the history of the generations of Perez: Perez became the father of Hezron,
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 and Hezron became the father of Ram, and Ram became the father of Amminadab,
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 and Amminadab became the father of Nahshon, and Nahshon became the father of Salmon,
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 and Salmon became the father of Boaz, and Boaz became the father of Obed,
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 and Obed became the father of Jesse, and Jesse became the father of David.
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >