< Psalms 86 >

1 A Prayer by David. Hear, Yahweh, and answer me, for I am poor and needy.
Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
2 Preserve my soul, for I am godly. You, my God, save your servant who trusts in you.
Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
3 Be merciful to me, Lord, for I call to you all day long.
Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
4 Bring joy to the soul of your servant, for to you, Lord, do I lift up my soul.
Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
5 For you, Lord, are good, and ready to forgive, abundant in loving kindness to all those who call on you.
Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
6 Hear, Yahweh, my prayer. Listen to the voice of my petitions.
Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
7 In the day of my trouble I will call on you, for you will answer me.
Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
8 There is no one like you among the gods, Lord, nor any deeds like your deeds.
Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
9 All nations you have made will come and worship before you, Lord. They shall glorify your name.
Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
10 For you are great, and do wondrous things. You are God alone.
Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
11 Teach me your way, Yahweh. I will walk in your truth. Make my heart undivided to fear your name.
Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
12 I will praise you, Lord my God, with my whole heart. I will glorify your name forever more.
Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
13 For your loving kindness is great toward me. You have delivered my soul from the lowest Sheol. (Sheol h7585)
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol h7585)
14 God, the proud have risen up against me. A company of violent men have sought after my soul, and they don’t hold regard for you before them.
Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
15 But you, Lord, are a merciful and gracious God, slow to anger, and abundant in loving kindness and truth.
Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
16 Turn to me, and have mercy on me! Give your strength to your servant. Save the son of your servant.
Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
17 Show me a sign of your goodness, that those who hate me may see it, and be shamed, because you, Yahweh, have helped me, and comforted me.
Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.

< Psalms 86 >