< Psalms 48 >

1 A Song. A Psalm by the sons of Korah. Great is Yahweh, and greatly to be praised, in the city of our God, in his holy mountain.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is Mount Zion, on the north sides, the city of the great King.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 God has shown himself in her citadels as a refuge.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 For, behold, the kings assembled themselves, they passed by together.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 They saw it, then they were amazed. They were dismayed. They hurried away.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Trembling took hold of them there, pain, as of a woman in travail.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 With the east wind, you break the ships of Tarshish.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 As we have heard, so we have seen, in the city of Yahweh of Armies, in the city of our God. God will establish it forever. (Selah)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 We have thought about your loving kindness, God, in the middle of your temple.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 As is your name, God, so is your praise to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Let Mount Zion be glad! Let the daughters of Judah rejoice because of your judgments.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Walk about Zion, and go around her. Number its towers.
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Notice her bulwarks. Consider her palaces, that you may tell it to the next generation.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< Psalms 48 >