< Psalms 19 >

1 For the Chief Musician. A Psalm by David. The heavens declare the glory of God. The expanse shows his handiwork.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 Day after day they pour out speech, and night after night they display knowledge.
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 There is no speech nor language where their voice is not heard.
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4 Their voice has gone out through all the earth, their words to the end of the world. In them he has set a tent for the sun,
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 which is as a bridegroom coming out of his room, like a strong man rejoicing to run his course.
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6 His going out is from the end of the heavens, his circuit to its ends. There is nothing hidden from its heat.
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
7 Yahweh’s law is perfect, restoring the soul. Yahweh’s covenant is sure, making wise the simple.
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
8 Yahweh’s precepts are right, rejoicing the heart. Yahweh’s commandment is pure, enlightening the eyes.
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
9 The fear of Yahweh is clean, enduring forever. Yahweh’s ordinances are true, and righteous altogether.
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
10 They are more to be desired than gold, yes, than much fine gold, sweeter also than honey and the extract of the honeycomb.
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
11 Moreover your servant is warned by them. In keeping them there is great reward.
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12 Who can discern his errors? Forgive me from hidden errors.
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13 Keep back your servant also from presumptuous sins. Let them not have dominion over me. Then I will be upright. I will be blameless and innocent of great transgression.
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
14 Let the words of my mouth and the meditation of my heart be acceptable in your sight, Yahweh, my rock, and my redeemer.
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

< Psalms 19 >