< Psalms 132 >

1 A Song of Ascents. Yahweh, remember David and all his affliction,
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 how he swore to Yahweh, and vowed to the Mighty One of Jacob:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 “Surely I will not come into the structure of my house, nor go up into my bed;
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 I will not give sleep to my eyes, or slumber to my eyelids,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 until I find out a place for Yahweh, a dwelling for the Mighty One of Jacob.”
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Behold, we heard of it in Ephrathah. We found it in the field of Jaar.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 “We will go into his dwelling place. We will worship at his footstool.”
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Arise, Yahweh, into your resting place, you, and the ark of your strength.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Let your priests be clothed with righteousness. Let your saints shout for joy!
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 For your servant David’s sake, don’t turn away the face of your anointed one.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Yahweh has sworn to David in truth. He will not turn from it: “I will set the fruit of your body on your throne.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 If your children will keep my covenant, my testimony that I will teach them, their children also will sit on your throne forever more.”
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 For Yahweh has chosen Zion. He has desired it for his habitation.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 “This is my resting place forever. I will live here, for I have desired it.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 I will abundantly bless her provision. I will satisfy her poor with bread.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 I will also clothe her priests with salvation. Her saints will shout aloud for joy.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 I will make the horn of David to bud there. I have ordained a lamp for my anointed.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 I will clothe his enemies with shame, but on himself, his crown will shine.”
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalms 132 >