< Psalms 120 >

1 A Song of Ascents. In my distress, I cried to Yahweh. He answered me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Deliver my soul, Yahweh, from lying lips, from a deceitful tongue.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 What will be given to you, and what will be done more to you, you deceitful tongue?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Sharp arrows of the mighty, with coals of juniper.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Woe is me, that I live in Meshech, that I dwell among the tents of Kedar!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 My soul has had her dwelling too long with him who hates peace.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 I am for peace, but when I speak, they are for war.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Psalms 120 >