< Proverbs 29 >

1 He who is often rebuked and stiffens his neck will be destroyed suddenly, with no remedy.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 When the righteous thrive, the people rejoice; but when the wicked rule, the people groan.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 Whoever loves wisdom brings joy to his father; but a companion of prostitutes squanders his wealth.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 The king by justice makes the land stable, but he who takes bribes tears it down.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 A man who flatters his neighbor spreads a net for his feet.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 An evil man is snared by his sin, but the righteous can sing and be glad.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 The righteous care about justice for the poor. The wicked aren’t concerned about knowledge.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Mockers stir up a city, but wise men turn away anger.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 If a wise man goes to court with a foolish man, the fool rages or scoffs, and there is no peace.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 The bloodthirsty hate a man of integrity; and they seek the life of the upright.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 A fool vents all of his anger, but a wise man brings himself under control.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 If a ruler listens to lies, all of his officials are wicked.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 The poor man and the oppressor have this in common: Yahweh gives sight to the eyes of both.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 The king who fairly judges the poor, his throne shall be established forever.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 The rod of correction gives wisdom, but a child left to himself causes shame to his mother.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 When the wicked increase, sin increases; but the righteous will see their downfall.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Correct your son, and he will give you peace; yes, he will bring delight to your soul.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Where there is no revelation, the people cast off restraint; but one who keeps the law is blessed.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 A servant can’t be corrected by words. Though he understands, yet he will not respond.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Do you see a man who is hasty in his words? There is more hope for a fool than for him.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 He who pampers his servant from youth will have him become a son in the end.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 An angry man stirs up strife, and a wrathful man abounds in sin.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 A man’s pride brings him low, but one of lowly spirit gains honor.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 Whoever is an accomplice of a thief is an enemy of his own soul. He takes an oath, but dares not testify.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 The fear of man proves to be a snare, but whoever puts his trust in Yahweh is kept safe.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Many seek the ruler’s favor, but a man’s justice comes from Yahweh.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 A dishonest man detests the righteous, and the upright in their ways detest the wicked.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Proverbs 29 >