< Philippians 4 >

1 Therefore, my brothers, beloved and longed for, my joy and crown, stand firm in the Lord in this way, my beloved.
Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
2 I exhort Euodia, and I exhort Syntyche, to think the same way in the Lord.
Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
3 Yes, I beg you also, true partner, help these women, for they labored with me in the Good News with Clement also, and the rest of my fellow workers, whose names are in the book of life.
Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
4 Rejoice in the Lord always! Again I will say, “Rejoice!”
Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
5 Let your gentleness be known to all men. The Lord is at hand.
Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
6 In nothing be anxious, but in everything, by prayer and petition with thanksgiving, let your requests be made known to God.
Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 And the peace of God, which surpasses all understanding, will guard your hearts and your thoughts in Christ Jesus.
Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
8 Finally, brothers, whatever things are true, whatever things are honorable, whatever things are just, whatever things are pure, whatever things are lovely, whatever things are of good report: if there is any virtue and if there is anything worthy of praise, think about these things.
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
9 Do the things which you learned, received, heard, and saw in me, and the God of peace will be with you.
Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
10 But I rejoice in the Lord greatly that now at length you have revived your thought for me; in which you did indeed take thought, but you lacked opportunity.
Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
11 Not that I speak because of lack, for I have learned in whatever state I am, to be content in it.
Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
12 I know how to be humbled, and I also know how to abound. In any and all circumstances I have learned the secret both to be filled and to be hungry, both to abound and to be in need.
Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
13 I can do all things through Christ who strengthens me.
Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
14 However you did well that you shared in my affliction.
Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
15 You yourselves also know, you Philippians, that in the beginning of the Good News, when I departed from Macedonia, no assembly shared with me in the matter of giving and receiving but you only.
Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
16 For even in Thessalonica you sent once and again to my need.
Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
17 Not that I seek for the gift, but I seek for the fruit that increases to your account.
Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
18 But I have all things and abound. I am filled, having received from Epaphroditus the things that came from you, a sweet-smelling fragrance, an acceptable and well-pleasing sacrifice to God.
Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
19 My God will supply every need of yours according to his riches in glory in Christ Jesus.
Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
20 Now to our God and Father be the glory forever and ever! Amen. (aiōn g165)
Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
21 Greet every saint in Christ Jesus. The brothers who are with me greet you.
Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
22 All the saints greet you, especially those who are of Caesar’s household.
Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
23 The grace of the Lord Jesus Christ be with you all. Amen.
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.

< Philippians 4 >