< Numbers 31 >

1 Yahweh spoke to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Avenge the children of Israel on the Midianites. Afterward you shall be gathered to your people.”
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 Moses spoke to the people, saying, “Arm men from among you for war, that they may go against Midian, to execute Yahweh’s vengeance on Midian.
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 You shall send one thousand out of every tribe, throughout all the tribes of Israel, to the war.”
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 So there were delivered, out of the thousands of Israel, a thousand from every tribe, twelve thousand armed for war.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 Moses sent them, one thousand of every tribe, to the war with Phinehas the son of Eleazar the priest, to the war, with the vessels of the sanctuary and the trumpets for the alarm in his hand.
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 They fought against Midian, as Yahweh commanded Moses. They killed every male.
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 They killed the kings of Midian with the rest of their slain: Evi, Rekem, Zur, Hur, and Reba, the five kings of Midian. They also killed Balaam the son of Beor with the sword.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 The children of Israel took the women of Midian captive with their little ones; and all their livestock, all their flocks, and all their goods, they took as plunder.
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 All their cities in the places in which they lived, and all their encampments, they burned with fire.
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 They took all the captives, and all the plunder, both of man and of animal.
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 They brought the captives with the prey and the plunder, to Moses, and to Eleazar the priest, and to the congregation of the children of Israel, to the camp at the plains of Moab, which are by the Jordan at Jericho.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 Moses and Eleazar the priest, with all the princes of the congregation, went out to meet them outside of the camp.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 Moses was angry with the officers of the army, the captains of thousands and the captains of hundreds, who came from the service of the war.
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 Moses said to them, “Have you saved all the women alive?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 Behold, these caused the children of Israel, through the counsel of Balaam, to commit trespass against Yahweh in the matter of Peor, and so the plague was among the congregation of Yahweh.
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 Now therefore kill every male among the little ones, and kill every woman who has known man by lying with him.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 But all the girls, who have not known man by lying with him, keep alive for yourselves.
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 “Encamp outside of the camp for seven days. Whoever has killed any person, and whoever has touched any slain, purify yourselves on the third day and on the seventh day, you and your captives.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 You shall purify every garment, and all that is made of skin, and all work of goats’ hair, and all things made of wood.”
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 Eleazar the priest said to the men of war who went to the battle, “This is the statute of the law which Yahweh has commanded Moses.
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 However the gold, and the silver, the bronze, the iron, the tin, and the lead,
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
23 everything that may withstand the fire, you shall make to go through the fire, and it shall be clean; nevertheless it shall be purified with the water for impurity. All that doesn’t withstand the fire you shall make to go through the water.
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 You shall wash your clothes on the seventh day, and you shall be clean. Afterward you shall come into the camp.”
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 Yahweh spoke to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
26 “Count the plunder that was taken, both of man and of animal, you, and Eleazar the priest, and the heads of the fathers’ households of the congregation;
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 and divide the plunder into two parts: between the men skilled in war, who went out to battle, and all the congregation.
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 Levy a tribute to Yahweh of the men of war who went out to battle: one soul of five hundred; of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks.
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 Take it from their half, and give it to Eleazar the priest, for Yahweh’s wave offering.
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 Of the children of Israel’s half, you shall take one drawn out of every fifty, of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks, of all the livestock, and give them to the Levites, who perform the duty of Yahweh’s tabernacle.”
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 Moses and Eleazar the priest did as Yahweh commanded Moses.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Now the plunder, over and above the booty which the men of war took, was six hundred seventy-five thousand sheep,
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
33 seventy-two thousand head of cattle,
ngʼombe 72,000,
34 sixty-one thousand donkeys,
punda 61,000,
35 and thirty-two thousand persons in all, of the women who had not known man by lying with him.
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 The half, which was the portion of those who went out to war, was in number three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep;
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
37 and Yahweh’s tribute of the sheep was six hundred seventy-five.
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
38 The cattle were thirty-six thousand, of which Yahweh’s tribute was seventy-two.
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
39 The donkeys were thirty thousand five hundred, of which Yahweh’s tribute was sixty-one.
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
40 The persons were sixteen thousand, of whom Yahweh’s tribute was thirty-two persons.
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 Moses gave the tribute, which was Yahweh’s wave offering, to Eleazar the priest, as Yahweh commanded Moses.
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 Of the children of Israel’s half, which Moses divided off from the men who fought
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
43 (now the congregation’s half was three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
44 thirty-six thousand head of cattle,
ngʼombe 36,000,
45 thirty thousand five hundred donkeys,
punda 30,500,
46 and sixteen thousand persons),
na wanadamu 16,000.
47 even of the children of Israel’s half, Moses took one drawn out of every fifty, both of man and of animal, and gave them to the Levites, who performed the duty of Yahweh’s tabernacle, as Yahweh commanded Moses.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 The officers who were over the thousands of the army, the captains of thousands, and the captains of hundreds, came near to Moses.
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 They said to Moses, “Your servants have taken the sum of the men of war who are under our command, and there lacks not one man of us.
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 We have brought Yahweh’s offering, what every man found: gold ornaments, armlets, bracelets, signet rings, earrings, and necklaces, to make atonement for our souls before Yahweh.”
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 Moses and Eleazar the priest took their gold, even all worked jewels.
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 All the gold of the wave offering that they offered up to Yahweh, of the captains of thousands, and of the captains of hundreds, was sixteen thousand seven hundred fifty shekels.
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 The men of war had taken booty, every man for himself.
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 Moses and Eleazar the priest took the gold of the captains of thousands and of hundreds, and brought it into the Tent of Meeting for a memorial for the children of Israel before Yahweh.
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Numbers 31 >