< Luke 20 >

1 On one of those days, as he was teaching the people in the temple and preaching the Good News, the priests and scribes came to him with the elders.
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 They asked him, “Tell us: by what authority do you do these things? Or who is giving you this authority?”
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 He answered them, “I also will ask you one question. Tell me:
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 the baptism of John, was it from heaven, or from men?”
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 They reasoned with themselves, saying, “If we say, ‘From heaven,’ he will say, ‘Why didn’t you believe him?’
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But if we say, ‘From men,’ all the people will stone us, for they are persuaded that John was a prophet.”
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 They answered that they didn’t know where it was from.
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 Jesus said to them, “Neither will I tell you by what authority I do these things.”
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 He began to tell the people this parable: “A man planted a vineyard and rented it out to some farmers, and went into another country for a long time.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 At the proper season, he sent a servant to the farmers to collect his share of the fruit of the vineyard. But the farmers beat him and sent him away empty.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 He sent yet another servant, and they also beat him and treated him shamefully, and sent him away empty.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 He sent yet a third, and they also wounded him and threw him out.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 The lord of the vineyard said, ‘What shall I do? I will send my beloved son. It may be that seeing him, they will respect him.’
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 “But when the farmers saw him, they reasoned among themselves, saying, ‘This is the heir. Come, let’s kill him, that the inheritance may be ours.’
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 Then they threw him out of the vineyard and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” When they heard that, they said, “May that never be!”
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 But he looked at them and said, “Then what is this that is written, ‘The stone which the builders rejected was made the chief cornerstone’?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Everyone who falls on that stone will be broken to pieces, but it will crush whomever it falls on to dust.”
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 The chief priests and the scribes sought to lay hands on him that very hour, but they feared the people—for they knew he had spoken this parable against them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 They watched him and sent out spies, who pretended to be righteous, that they might trap him in something he said, so as to deliver him up to the power and authority of the governor.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 They asked him, “Teacher, we know that you say and teach what is right, and aren’t partial to anyone, but truly teach the way of God.
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Is it lawful for us to pay taxes to Caesar, or not?”
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 But he perceived their craftiness, and said to them, “Why do you test me?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Show me a denarius. Whose image and inscription are on it?” They answered, “Caesar’s.”
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 He said to them, “Then give to Caesar the things that are Caesar’s, and to God the things that are God’s.”
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 They weren’t able to trap him in his words before the people. They marveled at his answer and were silent.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Some of the Sadducees came to him, those who deny that there is a resurrection.
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 They asked him, “Teacher, Moses wrote to us that if a man’s brother dies having a wife, and he is childless, his brother should take the wife and raise up children for his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 There were therefore seven brothers. The first took a wife, and died childless.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 The second took her as wife, and he died childless.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 The third took her, and likewise the seven all left no children, and died.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 Afterward the woman also died.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Therefore in the resurrection whose wife of them will she be? For the seven had her as a wife.”
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 Jesus said to them, “The children of this age marry and are given in marriage. (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 But those who are considered worthy to attain to that age and the resurrection from the dead neither marry nor are given in marriage. (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 For they can’t die any more, for they are like the angels and are children of God, being children of the resurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 But that the dead are raised, even Moses showed at the bush, when he called the Lord ‘The God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob.’
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 Now he is not the God of the dead, but of the living, for all are alive to him.”
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Some of the scribes answered, “Teacher, you speak well.”
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 They didn’t dare to ask him any more questions.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 He said to them, “Why do they say that the Christ is David’s son?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 David himself says in the book of Psalms, ‘The Lord said to my Lord, “Sit at my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 until I make your enemies the footstool of your feet.”’
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 “David therefore calls him Lord, so how is he his son?”
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 In the hearing of all the people, he said to his disciples,
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 “Beware of those scribes who like to walk in long robes, and love greetings in the marketplaces, the best seats in the synagogues, and the best places at feasts;
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 who devour widows’ houses, and for a pretense make long prayers. These will receive greater condemnation.”
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luke 20 >