< Joshua 19 >

1 The second lot came out for Simeon, even for the tribe of the children of Simeon according to their families. Their inheritance was in the middle of the inheritance of the children of Judah.
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 They had for their inheritance Beersheba (or Sheba), Moladah,
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Hazar Shual, Balah, Ezem,
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltolad, Bethul, Hormah,
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Ziklag, Beth Marcaboth, Hazar Susah,
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Beth Lebaoth, and Sharuhen; thirteen cities with their villages;
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Ain, Rimmon, Ether, and Ashan; four cities with their villages;
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 and all the villages that were around these cities to Baalath Beer, Ramah of the South. This is the inheritance of the tribe of the children of Simeon according to their families.
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 Out of the part of the children of Judah was the inheritance of the children of Simeon; for the portion of the children of Judah was too much for them. Therefore the children of Simeon had inheritance in the middle of their inheritance.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 The third lot came up for the children of Zebulun according to their families. The border of their inheritance was to Sarid.
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 Their border went up westward, even to Maralah, and reached to Dabbesheth. It reached to the brook that is before Jokneam.
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 It turned from Sarid eastward toward the sunrise to the border of Chisloth Tabor. It went out to Daberath, and went up to Japhia.
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 From there it passed along eastward to Gath Hepher, to Ethkazin; and it went out at Rimmon which stretches to Neah.
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 The border turned around it on the north to Hannathon; and it ended at the valley of Iphtah El;
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah, and Bethlehem: twelve cities with their villages.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 This is the inheritance of the children of Zebulun according to their families, these cities with their villages.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 The fourth lot came out for Issachar, even for the children of Issachar according to their families.
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Their border was to Jezreel, Chesulloth, Shunem,
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hapharaim, Shion, Anaharath,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabbith, Kishion, Ebez,
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remeth, Engannim, En Haddah, and Beth Pazzez.
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 The border reached to Tabor, Shahazumah, and Beth Shemesh. Their border ended at the Jordan: sixteen cities with their villages.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 This is the inheritance of the tribe of the children of Issachar according to their families, the cities with their villages.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 The fifth lot came out for the tribe of the children of Asher according to their families.
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Their border was Helkath, Hali, Beten, Achshaph,
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Allammelech, Amad, Mishal. It reached to Carmel westward, and to Shihorlibnath.
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 It turned toward the sunrise to Beth Dagon, and reached to Zebulun, and to the valley of Iphtah El northward to Beth Emek and Neiel. It went out to Cabul on the left hand,
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 and Ebron, Rehob, Hammon, and Kanah, even to great Sidon.
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 The border turned to Ramah, to the fortified city of Tyre; and the border turned to Hosah. It ended at the sea by the region of Achzib;
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 Ummah also, and Aphek, and Rehob: twenty-two cities with their villages.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 This is the inheritance of the tribe of the children of Asher according to their families, these cities with their villages.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 The sixth lot came out for the children of Naphtali, even for the children of Naphtali according to their families.
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Their border was from Heleph, from the oak in Zaanannim, Adami-nekeb, and Jabneel, to Lakkum. It ended at the Jordan.
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 The border turned westward to Aznoth Tabor, and went out from there to Hukkok. It reached to Zebulun on the south, and reached to Asher on the west, and to Judah at the Jordan toward the sunrise.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 The fortified cities were Ziddim, Zer, Hammath, Rakkath, Chinnereth,
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36 Adamah, Ramah, Hazor,
Adama, Rama, Hazori,
37 Kedesh, Edrei, En Hazor,
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Iron, Migdal El, Horem, Beth Anath, and Beth Shemesh; nineteen cities with their villages.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 This is the inheritance of the tribe of the children of Naphtali according to their families, the cities with their villages.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 The seventh lot came out for the tribe of the children of Dan according to their families.
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 The border of their inheritance was Zorah, Eshtaol, Irshemesh,
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Shaalabbin, Aijalon, Ithlah,
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 Elon, Timnah, Ekron,
Eloni, Timna, Ekroni,
44 Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jehud, Bene Berak, Gath Rimmon,
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Me Jarkon, and Rakkon, with the border opposite Joppa.
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 The border of the children of Dan went out beyond them; for the children of Dan went up and fought against Leshem, and took it, and struck it with the edge of the sword, and possessed it, and lived therein, and called Leshem, Dan, after the name of Dan their forefather.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 This is the inheritance of the tribe of the children of Dan according to their families, these cities with their villages.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 So they finished distributing the land for inheritance by its borders. The children of Israel gave an inheritance to Joshua the son of Nun among them.
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 According to Yahweh’s commandment, they gave him the city which he asked, even Timnathserah in the hill country of Ephraim; and he built the city, and lived there.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 These are the inheritances, which Eleazar the priest, Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers’ houses of the tribes of the children of Israel, distributed for inheritance by lot in Shiloh before Yahweh, at the door of the Tent of Meeting. So they finished dividing the land.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

< Joshua 19 >