< Joshua 12 >

1 Now these are the kings of the land, whom the children of Israel struck, and possessed their land beyond the Jordan toward the sunrise, from the valley of the Arnon to Mount Hermon, and all the Arabah eastward:
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Sihon king of the Amorites, who lived in Heshbon, and ruled from Aroer, which is on the edge of the valley of the Arnon, and the middle of the valley, and half Gilead, even to the river Jabbok, the border of the children of Ammon;
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 and the Arabah to the sea of Chinneroth, eastward, and to the sea of the Arabah, even the Salt Sea, eastward, the way to Beth Jeshimoth; and on the south, under the slopes of Pisgah:
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 and the border of Og king of Bashan, of the remnant of the Rephaim, who lived at Ashtaroth and at Edrei,
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 and ruled in Mount Hermon, and in Salecah, and in all Bashan, to the border of the Geshurites and the Maacathites, and half Gilead, the border of Sihon king of Heshbon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moses the servant of Yahweh and the children of Israel struck them. Moses the servant of Yahweh gave it for a possession to the Reubenites, and the Gadites, and the half-tribe of Manasseh.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 These are the kings of the land whom Joshua and the children of Israel struck beyond the Jordan westward, from Baal Gad in the valley of Lebanon even to Mount Halak, that goes up to Seir. Joshua gave it to the tribes of Israel for a possession according to their divisions;
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 in the hill country, and in the lowland, and in the Arabah, and in the slopes, and in the wilderness, and in the South; the Hittite, the Amorite, and the Canaanite, the Perizzite, the Hivite, and the Jebusite:
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 the king of Jericho, one; the king of Ai, which is beside Bethel, one;
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 the king of Jerusalem, one; the king of Hebron, one;
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 the king of Jarmuth, one; the king of Lachish, one;
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 the king of Eglon, one; the king of Gezer, one;
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 the king of Debir, one; the king of Geder, one;
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 the king of Hormah, one; the king of Arad, one;
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 the king of Libnah, one; the king of Adullam, one;
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 the king of Makkedah, one; the king of Bethel, one;
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 the king of Tappuah, one; the king of Hepher, one;
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 the king of Aphek, one; the king of Lassharon, one;
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 the king of Madon, one; the king of Hazor, one;
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 the king of Shimron Meron, one; the king of Achshaph, one;
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 the king of Taanach, one; the king of Megiddo, one;
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 the king of Kedesh, one; the king of Jokneam in Carmel, one;
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 the king of Dor in the height of Dor, one; the king of Goiim in Gilgal, one;
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 the king of Tirzah, one: all the kings thirty-one.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Joshua 12 >