< John 2 >

1 The third day, there was a wedding in Cana of Galilee. Jesus’ mother was there.
Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
2 Jesus also was invited, with his disciples, to the wedding.
Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
3 When the wine ran out, Jesus’ mother said to him, “They have no wine.”
Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
4 Jesus said to her, “Woman, what does that have to do with you and me? My hour has not yet come.”
Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
5 His mother said to the servants, “Whatever he says to you, do it.”
Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
6 Now there were six water pots of stone set there after the Jews’ way of purifying, containing two or three metretes apiece.
Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
7 Jesus said to them, “Fill the water pots with water.” So they filled them up to the brim.
Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
8 He said to them, “Now draw some out, and take it to the ruler of the feast.” So they took it.
Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
9 When the ruler of the feast tasted the water now become wine, and didn’t know where it came from (but the servants who had drawn the water knew), the ruler of the feast called the bridegroom
Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
10 and said to him, “Everyone serves the good wine first, and when the guests have drunk freely, then that which is worse. You have kept the good wine until now!”
kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
11 This beginning of his signs Jesus did in Cana of Galilee, and revealed his glory; and his disciples believed in him.
Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
12 After this, he went down to Capernaum, he, and his mother, his brothers, and his disciples; and they stayed there a few days.
Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
13 The Passover of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14 He found in the temple those who sold oxen, sheep, and doves, and the changers of money sitting.
Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
15 He made a whip of cords and drove all out of the temple, both the sheep and the oxen; and he poured out the changers’ money and overthrew their tables.
Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
16 To those who sold the doves, he said, “Take these things out of here! Don’t make my Father’s house a marketplace!”
Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
17 His disciples remembered that it was written, “Zeal for your house will eat me up.”
Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
18 The Jews therefore answered him, “What sign do you show us, seeing that you do these things?”
Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
19 Jesus answered them, “Destroy this temple, and in three days I will raise it up.”
Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
20 The Jews therefore said, “It took forty-six years to build this temple! Will you raise it up in three days?”
Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
21 But he spoke of the temple of his body.
Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
22 When therefore he was raised from the dead, his disciples remembered that he said this, and they believed the Scripture and the word which Jesus had said.
Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
23 Now when he was in Jerusalem at the Passover, during the feast, many believed in his name, observing his signs which he did.
Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
24 But Jesus didn’t entrust himself to them, because he knew everyone,
Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
25 and because he didn’t need for anyone to testify concerning man; for he himself knew what was in man.
Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.

< John 2 >