< Job 5 >

1 “Call now; is there any who will answer you? To which of the holy ones will you turn?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 For resentment kills the foolish man, and jealousy kills the simple.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 I have seen the foolish taking root, but suddenly I cursed his habitation.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 His children are far from safety. They are crushed in the gate. Neither is there any to deliver them,
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 whose harvest the hungry eat up, and take it even out of the thorns. The snare gapes for their substance.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 For affliction doesn’t come out of the dust, neither does trouble spring out of the ground;
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 but man is born to trouble, as the sparks fly upward.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 “But as for me, I would seek God. I would commit my cause to God,
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 who does great things that can’t be fathomed, marvelous things without number;
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 who gives rain on the earth, and sends waters on the fields;
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 so that he sets up on high those who are low, those who mourn are exalted to safety.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 He frustrates the plans of the crafty, so that their hands can’t perform their enterprise.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 He takes the wise in their own craftiness; the counsel of the cunning is carried headlong.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 They meet with darkness in the day time, and grope at noonday as in the night.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 But he saves from the sword of their mouth, even the needy from the hand of the mighty.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 So the poor has hope, and injustice shuts her mouth.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 “Behold, happy is the man whom God corrects. Therefore do not despise the chastening of the Almighty.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 For he wounds and binds up. He injures and his hands make whole.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 He will deliver you in six troubles; yes, in seven no evil will touch you.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 In famine he will redeem you from death; in war, from the power of the sword.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 You will be hidden from the scourge of the tongue, neither will you be afraid of destruction when it comes.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 You will laugh at destruction and famine, neither will you be afraid of the animals of the earth.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 For you will be allied with the stones of the field. The animals of the field will be at peace with you.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 You will know that your tent is in peace. You will visit your fold, and will miss nothing.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 You will know also that your offspring will be great, your offspring as the grass of the earth.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 You will come to your grave in a full age, like a shock of grain comes in its season.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Behold, we have researched it. It is so. Hear it, and know it for your good.”
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >