< Job 31 >

1 “I made a covenant with my eyes; how then should I look lustfully at a young woman?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what is the portion from God above, and the heritage from the Almighty on high?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Is it not calamity to the unrighteous, and disaster to the workers of iniquity?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Doesn’t he see my ways, and count all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 “If I have walked with falsehood, and my foot has hurried to deceit
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 (let me be weighed in an even balance, that God may know my integrity);
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 if my step has turned out of the way, if my heart walked after my eyes, if any defilement has stuck to my hands,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 then let me sow, and let another eat. Yes, let the produce of my field be rooted out.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 “If my heart has been enticed to a woman, and I have laid wait at my neighbor’s door,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 then let my wife grind for another, and let others sleep with her.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For that would be a heinous crime. Yes, it would be an iniquity to be punished by the judges,
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 for it is a fire that consumes to destruction, and would root out all my increase.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 “If I have despised the cause of my male servant or of my female servant, when they contended with me,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 what then will I do when God rises up? When he visits, what will I answer him?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Didn’t he who made me in the womb make him? Didn’t one fashion us in the womb?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 “If I have withheld the poor from their desire, or have caused the eyes of the widow to fail,
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 or have eaten my morsel alone, and the fatherless has not eaten of it
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (no, from my youth he grew up with me as with a father, I have guided her from my mother’s womb);
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 if I have seen any perish for want of clothing, or that the needy had no covering;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 if his heart hasn’t blessed me, if he hasn’t been warmed with my sheep’s fleece;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 if I have lifted up my hand against the fatherless, because I saw my help in the gate;
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 then let my shoulder fall from the shoulder blade, and my arm be broken from the bone.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For calamity from God is a terror to me. Because of his majesty, I can do nothing.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 “If I have made gold my hope, and have said to the fine gold, ‘You are my confidence;’
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 If I have rejoiced because my wealth was great, and because my hand had gotten much;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 if I have seen the sun when it shined, or the moon moving in splendor,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 and my heart has been secretly enticed, and my hand threw a kiss from my mouth;
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 this also would be an iniquity to be punished by the judges, for I would have denied the God who is above.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 “If I have rejoiced at the destruction of him who hated me, or lifted up myself when evil found him
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 (I have certainly not allowed my mouth to sin by asking his life with a curse);
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 if the men of my tent have not said, ‘Who can find one who has not been filled with his meat?’
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 (the foreigner has not camped in the street, but I have opened my doors to the traveler);
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 if like Adam I have covered my transgressions, by hiding my iniquity in my heart,
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 because I feared the great multitude, and the contempt of families terrified me, so that I kept silence, and didn’t go out of the door—
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 oh that I had one to hear me! Behold, here is my signature! Let the Almighty answer me! Let the accuser write my indictment!
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Surely I would carry it on my shoulder, and I would bind it to me as a crown.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 I would declare to him the number of my steps. I would go near to him like a prince.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my land cries out against me, and its furrows weep together;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 if I have eaten its fruits without money, or have caused its owners to lose their life,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 let briers grow instead of wheat, and stinkweed instead of barley.” The words of Job are ended.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >