< Job 18 >

1 Then Bildad the Shuhite answered,
Bildadi Mshuhi akajibu:
2 “How long will you hunt for words? Consider, and afterwards we will speak.
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3 Why are we counted as animals, which have become unclean in your sight?
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4 You who tear yourself in your anger, will the earth be forsaken for you? Or will the rock be removed out of its place?
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5 “Yes, the light of the wicked will be put out. The spark of his fire won’t shine.
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6 The light will be dark in his tent. His lamp above him will be put out.
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7 The steps of his strength will be shortened. His own counsel will cast him down.
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8 For he is cast into a net by his own feet, and he wanders into its mesh.
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 A snare will take him by the heel. A trap will catch him.
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 A noose is hidden for him in the ground, a trap for him on the path.
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11 Terrors will make him afraid on every side, and will chase him at his heels.
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12 His strength will be famished. Calamity will be ready at his side.
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 The members of his body will be devoured. The firstborn of death will devour his members.
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 He will be rooted out of the security of his tent. He will be brought to the king of terrors.
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 There will dwell in his tent that which is none of his. Sulfur will be scattered on his habitation.
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16 His roots will be dried up beneath. His branch will be cut off above.
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17 His memory will perish from the earth. He will have no name in the street.
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18 He will be driven from light into darkness, and chased out of the world.
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19 He will have neither son nor grandson among his people, nor any remaining where he lived.
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20 Those who come after will be astonished at his day, as those who went before were frightened.
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21 Surely such are the dwellings of the unrighteous. This is the place of him who doesn’t know God.”
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

< Job 18 >