< Genesis 7 >

1 Yahweh said to Noah, “Come with all of your household into the ship, for I have seen your righteousness before me in this generation.
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 You shall take seven pairs of every clean animal with you, the male and his female. Of the animals that are not clean, take two, the male and his female.
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 Also of the birds of the sky, seven and seven, male and female, to keep seed alive on the surface of all the earth.
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 In seven days, I will cause it to rain on the earth for forty days and forty nights. I will destroy every living thing that I have made from the surface of the ground.”
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5 Noah did everything that Yahweh commanded him.
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6 Noah was six hundred years old when the flood of waters came on the earth.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 Noah went into the ship with his sons, his wife, and his sons’ wives, because of the floodwaters.
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 Clean animals, unclean animals, birds, and everything that creeps on the ground
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 went by pairs to Noah into the ship, male and female, as God commanded Noah.
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10 After the seven days, the floodwaters came on the earth.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 In the six hundredth year of Noah’s life, in the second month, on the seventeenth day of the month, on that day all the fountains of the great deep burst open, and the sky’s windows opened.
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
12 It rained on the earth forty days and forty nights.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 In the same day Noah, and Shem, Ham, and Japheth—the sons of Noah—and Noah’s wife and the three wives of his sons with them, entered into the ship—
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 they, and every animal after its kind, all the livestock after their kind, every creeping thing that creeps on the earth after its kind, and every bird after its kind, every bird of every sort.
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 Pairs from all flesh with the breath of life in them went into the ship to Noah.
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 Those who went in, went in male and female of all flesh, as God commanded him; then Yahweh shut him in.
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 The flood was forty days on the earth. The waters increased, and lifted up the ship, and it was lifted up above the earth.
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
18 The waters rose, and increased greatly on the earth; and the ship floated on the surface of the waters.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 The waters rose very high on the earth. All the high mountains that were under the whole sky were covered.
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
20 The waters rose fifteen cubits higher, and the mountains were covered.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 All flesh died that moved on the earth, including birds, livestock, animals, every creeping thing that creeps on the earth, and every man.
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
22 All on the dry land, in whose nostrils was the breath of the spirit of life, died.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 Every living thing was destroyed that was on the surface of the ground, including man, livestock, creeping things, and birds of the sky. They were destroyed from the earth. Only Noah was left, and those who were with him in the ship.
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
24 The waters flooded the earth one hundred fifty days.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.

< Genesis 7 >

The Great Flood
The Great Flood