< Genesis 5 >

1 This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, he made him in God’s likeness.
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 He created them male and female, and blessed them. On the day they were created, he named them Adam.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Adam lived one hundred thirty years, and became the father of a son in his own likeness, after his image, and named him Seth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 The days of Adam after he became the father of Seth were eight hundred years, and he became the father of other sons and daughters.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 All the days that Adam lived were nine hundred thirty years, then he died.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Seth lived one hundred five years, then became the father of Enosh.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Seth lived after he became the father of Enosh eight hundred seven years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 All of the days of Seth were nine hundred twelve years, then he died.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Enosh lived ninety years, and became the father of Kenan.
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Enosh lived after he became the father of Kenan eight hundred fifteen years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 All of the days of Enosh were nine hundred five years, then he died.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Kenan lived seventy years, then became the father of Mahalalel.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Kenan lived after he became the father of Mahalalel eight hundred forty years, and became the father of other sons and daughters
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 and all of the days of Kenan were nine hundred ten years, then he died.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Mahalalel lived sixty-five years, then became the father of Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 Mahalalel lived after he became the father of Jared eight hundred thirty years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 All of the days of Mahalalel were eight hundred ninety-five years, then he died.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 Jared lived one hundred sixty-two years, then became the father of Enoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 Jared lived after he became the father of Enoch eight hundred years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 All of the days of Jared were nine hundred sixty-two years, then he died.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Enoch lived sixty-five years, then became the father of Methuselah.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 After Methuselah’s birth, Enoch walked with God for three hundred years, and became the father of more sons and daughters.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 All the days of Enoch were three hundred sixty-five years.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 Enoch walked with God, and he was not found, for God took him.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Methuselah lived one hundred eighty-seven years, then became the father of Lamech.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 Methuselah lived after he became the father of Lamech seven hundred eighty-two years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 All the days of Methuselah were nine hundred sixty-nine years, then he died.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Lamech lived one hundred eighty-two years, then became the father of a son.
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 He named him Noah, saying, “This one will comfort us in our work and in the toil of our hands, caused by the ground which Yahweh has cursed.”
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 Lamech lived after he became the father of Noah five hundred ninety-five years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 All the days of Lamech were seven hundred seventy-seven years, then he died.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 Noah was five hundred years old, then Noah became the father of Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< Genesis 5 >