< Ephesians 3 >

1 For this cause I, Paul, am the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles,
Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
2 if it is so that you have heard of the administration of that grace of God which was given me toward you,
Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
3 how that by revelation the mystery was made known to me, as I wrote before in few words,
Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
4 by which, when you read, you can perceive my understanding in the mystery of Christ,
Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
5 which in other generations was not made known to the children of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in the Spirit,
Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
6 that the Gentiles are fellow heirs and fellow members of the body, and fellow partakers of his promise in Christ Jesus through the Good News,
Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
7 of which I was made a servant according to the gift of that grace of God which was given me according to the working of his power.
Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
8 To me, the very least of all saints, was this grace given, to preach to the Gentiles the unsearchable riches of Christ,
Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
9 and to make all men see what is the administration of the mystery which for ages has been hidden in God, who created all things through Jesus Christ, (aiōn g165)
inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn g165)
10 to the intent that now through the assembly the manifold wisdom of God might be made known to the principalities and the powers in the heavenly places,
Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
11 according to the eternal purpose which he accomplished in Christ Jesus our Lord. (aiōn g165)
Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
12 In him we have boldness and access in confidence through our faith in him.
Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
13 Therefore I ask that you may not lose heart at my troubles for you, which are your glory.
Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
14 For this cause, I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
15 from whom every family in heaven and on earth is named,
ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
16 that he would grant you, according to the riches of his glory, that you may be strengthened with power through his Spirit in the inner person,
Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
17 that Christ may dwell in your hearts through faith, to the end that you, being rooted and grounded in love,
Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
18 may be strengthened to comprehend with all the saints what is the width and length and height and depth,
Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
19 and to know Christ’s love which surpasses knowledge, that you may be filled with all the fullness of God.
Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
20 Now to him who is able to do exceedingly abundantly above all that we ask or think, according to the power that works in us,
Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
21 to him be the glory in the assembly and in Christ Jesus to all generations, forever and ever. Amen. (aiōn g165)
kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn g165)

< Ephesians 3 >