< Colossians 3 >

1 If then you were raised together with Christ, seek the things that are above, where Christ is, seated on the right hand of God.
Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
2 Set your mind on the things that are above, not on the things that are on the earth.
Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
3 For you died, and your life is hidden with Christ in God.
Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 When Christ, our life, is revealed, then you will also be revealed with him in glory.
Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
5 Put to death therefore your members which are on the earth: sexual immorality, uncleanness, depraved passion, evil desire, and covetousness, which is idolatry.
Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
6 For these things’ sake the wrath of God comes on the children of disobedience.
Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
7 You also once walked in those, when you lived in them,
Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
8 but now you must put them all away: anger, wrath, malice, slander, and shameful speaking out of your mouth.
Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
9 Don’t lie to one another, seeing that you have put off the old man with his doings,
Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
10 and have put on the new man, who is being renewed in knowledge after the image of his Creator,
Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
11 where there can’t be Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, bondservant, or free person; but Christ is all, and in all.
Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
12 Put on therefore, as God’s chosen ones, holy and beloved, a heart of compassion, kindness, lowliness, humility, and perseverance;
Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 bearing with one another, and forgiving each other, if any man has a complaint against any; even as Christ forgave you, so you also do.
Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
14 Above all these things, walk in love, which is the bond of perfection.
Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
15 And let the peace of God rule in your hearts, to which also you were called in one body, and be thankful.
Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
16 Let the word of Christ dwell in you richly; in all wisdom teaching and admonishing one another with psalms, hymns, and spiritual songs, singing with grace in your heart to the Lord.
Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
17 Whatever you do, in word or in deed, do all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father through him.
Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
18 Wives, be in subjection to your husbands, as is fitting in the Lord.
Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
19 Husbands, love your wives, and don’t be bitter against them.
Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
20 Children, obey your parents in all things, for this pleases the Lord.
Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
21 Fathers, don’t provoke your children, so that they won’t be discouraged.
Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
22 Servants, obey in all things those who are your masters according to the flesh, not just when they are looking, as men pleasers, but in singleness of heart, fearing God.
Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
23 And whatever you do, work heartily, as for the Lord and not for men,
Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
24 knowing that from the Lord you will receive the reward of the inheritance; for you serve the Lord Christ.
Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
25 But he who does wrong will receive again for the wrong that he has done, and there is no partiality.
Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.

< Colossians 3 >