< 1 Timothy 2 >

1 I exhort therefore, first of all, that petitions, prayers, intercessions, and givings of thanks be made for all men,
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 for kings and all who are in high places, that we may lead a tranquil and quiet life in all godliness and reverence.
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 For this is good and acceptable in the sight of God our Savior,
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 who desires all people to be saved and come to full knowledge of the truth.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 For there is one God and one mediator between God and men, the man Christ Jesus,
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 who gave himself as a ransom for all, the testimony at the proper time,
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 to which I was appointed a preacher and an apostle—I am telling the truth in Christ, not lying—a teacher of the Gentiles in faith and truth.
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 I desire therefore that the men in every place pray, lifting up holy hands without anger and doubting.
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 In the same way, that women also adorn themselves in decent clothing, with modesty and propriety, not with braided hair, gold, pearls, or expensive clothing,
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 but with good works, which is appropriate for women professing godliness.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 Let a woman learn in quietness with full submission.
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 But I don’t permit a woman to teach, nor to exercise authority over a man, but to be in quietness.
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 For Adam was formed first, then Eve.
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 Adam wasn’t deceived, but the woman, being deceived, has fallen into disobedience;
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 but she will be saved through her childbearing, if they continue in faith, love, and holiness with sobriety.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

< 1 Timothy 2 >