< 1 Chronicles 14 >

1 Hiram king of Tyre sent messengers to David with cedar trees, masons, and carpenters, to build him a house.
Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
2 David perceived that Yahweh had established him king over Israel, for his kingdom was highly exalted, for his people Israel’s sake.
Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
3 David took more wives in Jerusalem, and David became the father of more sons and daughters.
Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
4 These are the names of the children whom he had in Jerusalem: Shammua, Shobab, Nathan, Solomon,
Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5 Ibhar, Elishua, Elpelet,
Ibihari, Elishua, Elpeleti,
6 Nogah, Nepheg, Japhia,
Noga, Nefegi, Yafia,
7 Elishama, Beeliada, and Eliphelet.
Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8 When the Philistines heard that David was anointed king over all Israel, all the Philistines went up to seek David; and David heard of it, and went out against them.
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
9 Now the Philistines had come and made a raid in the valley of Rephaim.
Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
10 David inquired of God, saying, “Shall I go up against the Philistines? Will you deliver them into my hand?” Yahweh said to him, “Go up; for I will deliver them into your hand.”
Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
11 So they came up to Baal Perazim, and David defeated them there. David said, God has broken my enemies by my hand, like waters breaking out. Therefore they called the name of that place Baal Perazim.
Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
12 They left their gods there; and David gave a command, and they were burned with fire.
Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
13 The Philistines made another raid in the valley.
Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
14 David inquired again of God; and God said to him, “You shall not go up after them. Turn away from them, and come on them opposite the mulberry trees.
hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
15 When you hear the sound of marching in the tops of the mulberry trees, then go out to battle; for God has gone out before you to strike the army of the Philistines.”
Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
16 David did as God commanded him; and they attacked the army of the Philistines from Gibeon even to Gezer.
Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
17 The fame of David went out into all lands; and Yahweh brought the fear of him on all nations.
Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.

< 1 Chronicles 14 >