< 1 Chronicles 11 >

1 Then all Israel gathered themselves to David to Hebron, saying, “Behold, we are your bone and your flesh.
Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
2 In times past, even when Saul was king, it was you who led out and brought in Israel. Yahweh your God said to you, ‘You shall be shepherd of my people Israel, and you shall be prince over my people Israel.’”
Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
3 So all the elders of Israel came to the king to Hebron; and David made a covenant with them in Hebron before Yahweh. They anointed David king over Israel, according to Yahweh’s word by Samuel.
Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
4 David and all Israel went to Jerusalem (also called Jebus); and the Jebusites, the inhabitants of the land, were there.
Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
5 The inhabitants of Jebus said to David, “You will not come in here!” Nevertheless David took the stronghold of Zion. The same is David’s city.
wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
6 David had said, “Whoever strikes the Jebusites first shall be chief and captain.” Joab the son of Zeruiah went up first, and was made chief.
Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
7 David lived in the stronghold; therefore they called it David’s city.
Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
8 He built the city all around, from Millo even around; and Joab repaired the rest of the city.
Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
9 David grew greater and greater, for Yahweh of Armies was with him.
Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
10 Now these are the chief of the mighty men whom David had, who showed themselves strong with him in his kingdom, together with all Israel, to make him king, according to Yahweh’s word concerning Israel.
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
11 This is the number of the mighty men whom David had: Jashobeam, the son of a Hachmonite, the chief of the thirty; he lifted up his spear against three hundred and killed them at one time.
Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
12 After him was Eleazar the son of Dodo, the Ahohite, who was one of the three mighty men.
Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
13 He was with David at Pasdammim, and there the Philistines were gathered together to battle, where there was a plot of ground full of barley; and the people fled from before the Philistines.
Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
14 They stood in the middle of the plot, defended it, and killed the Philistines; and Yahweh saved them by a great victory.
Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
15 Three of the thirty chief men went down to the rock to David, into the cave of Adullam; and the army of the Philistines were encamped in the valley of Rephaim.
Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
16 David was then in the stronghold, and the garrison of the Philistines was in Bethlehem at that time.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
17 David longed, and said, “Oh, that someone would give me water to drink from the well of Bethlehem, which is by the gate!”
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
18 The three broke through the army of the Philistines, and drew water out of the well of Bethlehem that was by the gate, took it, and brought it to David; but David would not drink any of it, but poured it out to Yahweh,
Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
19 and said, “My God forbid me, that I should do this! Shall I drink the blood of these men who have put their lives in jeopardy?” For they risked their lives to bring it. Therefore he would not drink it. The three mighty men did these things.
Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
20 Abishai, the brother of Joab, was chief of the three; for he lifted up his spear against three hundred and killed them, and had a name among the three.
Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
21 Of the three, he was more honorable than the two, and was made their captain; however he wasn’t included in the three.
Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
22 Benaiah the son of Jehoiada, the son of a valiant man of Kabzeel, who had done mighty deeds, killed the two sons of Ariel of Moab. He also went down and killed a lion in the middle of a pit on a snowy day.
Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
23 He killed an Egyptian, a man of great stature, five cubits high. In the Egyptian’s hand was a spear like a weaver’s beam; and he went down to him with a staff, plucked the spear out of the Egyptian’s hand, and killed him with his own spear.
Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
24 Benaiah the son of Jehoiada did these things and had a name among the three mighty men.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
25 Behold, he was more honorable than the thirty, but he didn’t attain to the three; and David set him over his guard.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
26 The mighty men of the armies also include Asahel the brother of Joab, Elhanan the son of Dodo of Bethlehem,
Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
27 Shammoth the Harorite, Helez the Pelonite,
Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
28 Ira the son of Ikkesh the Tekoite, Abiezer the Anathothite,
Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
29 Sibbecai the Hushathite, Ilai the Ahohite,
Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
30 Maharai the Netophathite, Heled the son of Baanah the Netophathite,
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
31 Ithai the son of Ribai of Gibeah of the children of Benjamin, Benaiah the Pirathonite,
Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
32 Hurai of the brooks of Gaash, Abiel the Arbathite,
Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
33 Azmaveth the Baharumite, Eliahba the Shaalbonite,
Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 the sons of Hashem the Gizonite, Jonathan the son of Shagee the Hararite,
wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
35 Ahiam the son of Sacar the Hararite, Eliphal the son of Ur,
Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
36 Hepher the Mecherathite, Ahijah the Pelonite,
Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
37 Hezro the Carmelite, Naarai the son of Ezbai,
Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
38 Joel the brother of Nathan, Mibhar the son of Hagri,
Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
39 Zelek the Ammonite, Naharai the Berothite (the armor bearer of Joab the son of Zeruiah),
Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
40 Ira the Ithrite, Gareb the Ithrite,
Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
41 Uriah the Hittite, Zabad the son of Ahlai,
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
42 Adina the son of Shiza the Reubenite (a chief of the Reubenites), and thirty with him,
Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
43 Hanan the son of Maacah, Joshaphat the Mithnite,
Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
44 Uzzia the Ashterathite, Shama and Jeiel the sons of Hotham the Aroerite,
Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
45 Jediael the son of Shimri, and Joha his brother, the Tizite,
Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
46 Eliel the Mahavite, and Jeribai, and Joshaviah, the sons of Elnaam, and Ithmah the Moabite,
Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
47 Eliel, Obed, and Jaasiel the Mezobaite.
Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.

< 1 Chronicles 11 >