< Luke 1 >

1 Many have taken on the work of putting together an account of the things that have been fulfilled among us,
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 just as they were passed down to us by those who from the first were eyewitnesses and servants of the word.
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 So it seemed good to me also, because I have accurately investigated everything from the beginning, to write an orderly account for you, most excellent Theophilus,
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 so that you might know the certainty of the things you have been taught.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 In the days of Herod, king of Judea, there was a certain priest named Zechariah, from the division of Abijah. His wife was from the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 They were both righteous before God, obeying all the commandments and ordinances of the Lord.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 But they had no child, because Elizabeth was barren, and they were both very old by this time.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now it came about that Zechariah was in God's presence, carrying out the priestly duties in the order of his division.
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 According to the customary way of choosing which priest would serve, he had been chosen by lot to enter into the temple of the Lord to burn incense.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 The whole crowd of people was praying outside at the hour when the incense was burned.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Now an angel of the Lord appeared to him and stood at the right side of the incense altar.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 When Zechariah saw him, he was terrified and fear fell on him.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 But the angel said to him, “Do not be afraid, Zechariah, because your prayer has been heard. Your wife Elizabeth will bear you a son. You will call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 You will have joy and gladness, and many will rejoice at his birth.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 For he will be great in the sight of the Lord. He must never drink wine or strong drink, and he will be filled with the Holy Spirit from his mother's womb.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 Many of the people of Israel will be turned to the Lord their God.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 He will go before the face of the Lord in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of the fathers to the children and the disobedient to the wisdom of the righteous—to make ready for the Lord a people prepared for him.”
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 Zechariah said to the angel, “How can I know this? For I am an old man and my wife is very old.”
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 The angel answered and said to him, “I am Gabriel, who stands in the presence of God. I was sent to speak to you, to bring you this good news.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 Behold! You will be silent, unable to speak, until the day these things take place. This is because you did not believe my words, which will be fulfilled at the right time.”
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 Now the people were waiting for Zechariah. They were surprised that he was spending so much time in the temple.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 But when he came out, he could not speak to them. They realized that he had seen a vision while he was in the temple. He kept on making signs to them and remained silent.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 It came about that when the days of his service were over, he went to his house.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 After these days, his wife Elizabeth conceived and for five months she kept herself hidden. She said,
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 “This is what the Lord has done for me when he looked at me with favor in order to take away my shame before people.”
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 In the sixth month, the angel Gabriel was sent from God to a city in Galilee named Nazareth,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 to a virgin engaged to a man whose name was Joseph. He belonged to the house of David, and the virgin's name was Mary.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 He came to her and said, “Greetings, you who are highly favored! The Lord is with you.”
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 But she was very confused by his words and she wondered what kind of greeting this could be.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 The angel said to her, “Do not be afraid, Mary, for you have found favor with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 See, you will conceive in your womb and bear a son. You will call his name 'Jesus.'
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 He will be great and will be called the Son of the Most High. The Lord God will give him the throne of his ancestor David.
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 He will reign over the house of Jacob forever, and there will be no end to his kingdom.” (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 Mary said to the angel, “How will this happen, since I have not slept with any man?”
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 The angel answered and said to her, “The Holy Spirit will come upon you, and the power of the Most High will come over you. So the holy one to be born will be called the Son of God.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 See, your relative Elizabeth has also conceived a son in her old age. This is the sixth month for her, she who was called barren.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 For nothing will be impossible for God.”
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Mary said, “See, I am the female servant of the Lord. Let it be for me according to your message.” Then the angel left her.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Then Mary arose in those days and quickly went into the hill country, to a city in Judea.
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 She went into the house of Zechariah and greeted Elizabeth.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 Now it happened that when Elizabeth heard Mary's greeting, the baby in her womb jumped, and Elizabeth was filled with the Holy Spirit.
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 She raised her voice and said loudly, “Blessed are you among women, and blessed is the fruit of your womb.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 Why has it happened to me that the mother of my Lord should come to me?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 For see, when the sound of your greeting came to my ears, the baby in my womb jumped for joy.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 Blessed is she who believed that there would be a fulfillment of the things that were told her from the Lord.”
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Mary said, “My soul praises the Lord,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 and my spirit has rejoiced in God my savior.
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 For he has looked at the low condition of his female servant. For see, from now on all generations will call me blessed.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 For he who is mighty has done great things for me, and his name is holy.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 His mercy lasts from generation to generation for those who fear him.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 He has displayed strength with his arm; he has scattered those who were proud about the thoughts of their hearts.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 He has thrown down princes from their thrones and he has raised up those of low condition.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 He has filled the hungry with good things, but the rich he has sent away empty.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He has given help to Israel his servant, so as to remember to show mercy
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 (as he said to our fathers) to Abraham and his descendants forever.” (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 Mary stayed with Elizabeth about three months and then returned to her house.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Now the time had come for Elizabeth to deliver her baby and she gave birth to a son.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 Her neighbors and her relatives heard that the Lord had shown his great mercy to her, and they rejoiced with her.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 Now it happened on the eighth day that they came to circumcise the child. They would have called him “Zechariah,” after the name of his father.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 But his mother answered and said, “No. He will be called John.”
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 They said to her, “There is no one among your relatives who is called by this name.”
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 They made signs to his father as to how he wanted him to be named.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 His father asked for a writing tablet and wrote, “His name is John.” They all were astonished at this.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Immediately his mouth was opened and his tongue was freed. He spoke and praised God.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 Fear came on all who lived around them. All these matters were spread throughout all the hill country of Judea.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 All who heard them stored them in their hearts, saying, “What then will this child become?” For the hand of the Lord was with him.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 His father Zechariah was filled with the Holy Spirit and prophesied, saying,
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 “Praised be the Lord, the God of Israel, for he has come to help and he has accomplished redemption for his people.
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 He has raised up a horn of salvation for us in the house of his servant David
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 (as he spoke by the mouth of his holy prophets from long ago), (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 salvation from our enemies and from the hand of all who hate us.
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 He will do this to show mercy to our fathers and to remember his holy covenant,
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 the oath that he spoke to Abraham our father.
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 He swore to grant to us that we, having been delivered out of the hand of our enemies, would serve him without fear,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 in holiness and righteousness before him all our days.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 Yes, and you, child, will be called a prophet of the Most High, for you will go before the face of the Lord to prepare his paths, to prepare people for his coming,
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 to give knowledge of salvation to his people by the forgiveness of their sins.
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 This will happen because of the tender mercy of our God, because of which the sunrise from on high will come to help us,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 to shine on those who sit in darkness and in the shadow of death. He will do this to guide our feet into the path of peace.”
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 Now the child grew and became strong in spirit, and he was in the wilderness until the day of his public appearance to Israel.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luke 1 >