< Titus 3 >

1 Remind your hearers to respect and obey the Powers that be, to be ready for every kind of good work, to speak ill of no one, to avoid quarrelling,
Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
2 to be forbearing, and under all circumstances to show a gentle spirit in dealing with others, whoever they may be.
Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
3 There was, you remember, a time when we ourselves were foolish, disobedient, misled, slaves to all kinds of passions and vices, living in a spirit of malice and envy, detested ourselves and hating one another.
Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
4 But, when the kindness of God our Saviour and his love for man were revealed, he saved us,
Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
5 not as the result of any righteous actions that we had done, but in fulfilment of his merciful purposes. He saved us by that Washing which was a New Birth to us, and by the renewing power of the Holy Spirit,
alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
6 which he poured out upon us abundantly through Jesus Christ our Saviour;
Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
7 that, having been pronounced righteous through his loving-kindness, we might enter on our inheritance with the hope of Immortal Life. (aiōnios g166)
ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios g166)
8 How true that saying is! And it is on these subjects that I desire you to lay especial stress, so that those who have learned to trust in God may be careful to devote themselves to doing good. Such subjects are excellent in themselves, and of real use to mankind.
Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
9 But have nothing to do with foolish discussions, or with genealogies, or with controversy, or disputes about the Law. They are useless and futile.
Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
10 If a man is causing divisions among you, after warning him once or twice, have nothing more to say to him.
Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
11 You may be sure that such a man has forsaken the Truth and is in the wrong; he stands self-condemned.
Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
12 As soon as I send Artemas or Tychicus to you, join me as quickly as possible at Nicopolis, for I have arranged to spend the winter there.
Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13 Do your best to help Zenas, the Teacher of the Law, and Apollos, on their way, and see that they want for nothing.
Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
14 Let all our People learn to devote themselves to doing good, so as to meet the most pressing needs, and that their lives may not be unfruitful.
Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
15 All who are with me here send you their greeting. Give my greeting to our friends in the Faith. God bless you all.
Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.

< Titus 3 >