< Luke 19 >

1 Then Jesus entered Jericho and was passing through.
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 And behold, there was a man named Zacchaeus. He was a chief tax collector, who was rich.
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He was trying to see who Jesus was, but he could not do so because of the crowd, for he was small in stature.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 So he ran on ahead and climbed a sycamore tree so that he could see him, because Jesus was about to pass by that way.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 When Jesus came to that place, he looked up and saw him. Then he said to him, “Zacchaeus, hurry and come down, for I must stay at yoʋr house today.”
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 So he hurried down and received Jesus with joy.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 When all the people saw it, they grumbled, saying, “He has gone in to stay with a sinful man.”
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 But Zacchaeus stood there and said to the Lord, “Behold, half of my goods, Lord, I give to the poor, and if I have extorted anything from anyone, I will pay back four times the amount.”
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 Jesus said to him, “Today salvation has come to this house, for this man also is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 For the Son of Man came to seek and save the lost.”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 Now as the people were listening to this, Jesus went on to tell a parable, because he was near Jerusalem, and because they thought that the kingdom of God was going to appear at once.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 So he said, “A man of noble birth went to a distant country to receive a kingdom for himself and then return.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 Calling ten of his servants, he gave them ten minas and said to them, ‘Engage in business until I come.’
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 Now his citizens hated him and sent a delegation after him, saying, ‘We do not want this man to reign over us.’
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 When he returned after receiving the kingdom, he summoned the servants to whom he had given the money, so that he might know who had gained what by engaging in business.
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 The first came before him and said, ‘Master, yoʋr mina has made ten minas more.’
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 The king said to him, ‘Well done, good servant! Because yoʋ have been faithful in a very small matter, take authority over ten cities.’
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 The second came and said, ‘Master, yoʋr mina has made five minas.’
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 The king said to him, ‘Yoʋ are to be over five cities.’
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 Another came and said, ‘Master, behold, here is yoʋr mina, which I kept put away in a piece of cloth.
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 For I was afraid of yoʋ, because yoʋ are a stern man. Yoʋ take out what yoʋ did not put in, and yoʋ reap what yoʋ did not sow.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 The king said to him, ‘I will condemn yoʋ by the words coming out of yoʋr own mouth, yoʋ evil servant. Yoʋ knew, did yoʋ, that I was a stern man, taking out what I did not put in, and reaping what I did not sow?
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 Why then did yoʋ not deposit my money in the bank, and when I came I would have collected it with interest?’
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 Then he said to those standing nearby, ‘Take the mina from him and give it to the one who has ten minas.’
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 (But they said to him, ‘Master, he has ten minas!’)
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 ‘For I tell you that everyone who has will be given more, but the one who does not have, even what he has will be taken away from him.
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But as for those enemies of mine who did not want me to reign over them, bring them here and slay them in front of me.’”
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 After saying these things, Jesus continued on his way up to Jerusalem, walking ahead of his disciples.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 As he drew near to Bethsphage and Bethany, at the mount called Olivet, he sent two of his disciples ahead,
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying, “Go into the village ahead of you. As you enter it, you will find a colt tied, on which no one has ever sat. Untie it and bring it here.
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 If anyone asks you, ‘Why are you untying it?’ tell him this: ‘The Lord has need of it.’”
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 So those who were sent went off and found it just as he had told them.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 As they were untying the colt, its owners said to them, “Why are you untying the colt?”
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 They said, “The Lord has need of it.”
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 Then they brought the colt to Jesus, threw their garments over it, and set Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 As he went along, people were spreading their garments on the road.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And as he drew near to the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to praise God joyfully with a loud voice for all the miracles they had seen,
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 saying, “Blessed is the king who comes in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory in the highest!”
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 But some of the Pharisees from among the crowd said to Jesus, “Teacher, rebuke yoʋr disciples.”
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 In response he said to them, “I tell you, if they keep silent, the stones will cry out.”
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 As he drew near to Jerusalem and saw the city, he wept over it,
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 saying, “If only yoʋ had known, especially on this yoʋr day, what would bring about yoʋr peace! But now it is hidden from yoʋr eyes.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the days will come upon yoʋ when yoʋr enemies build a barricade around yoʋ and encircle yoʋ, hemming yoʋ in on every side.
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 They will raze yoʋ to the ground, and yoʋr children within yoʋ. They will not leave in yoʋ one stone upon another, because yoʋ did not recognize the time of yoʋr visitation.”
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 Then Jesus entered the temple courts and began driving out those who were selling and buying there.
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 He said to them, “It is written, ‘My house is a house of prayer,’ but you have made it a den of robbers.”
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 Every day Jesus was teaching in the temple courts, but the chief priests and the scribes were seeking to destroy him, and so were the prominent leaders among the people.
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 But they could not figure out what to do, for all the people were hanging on his every word as they listened to him.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luke 19 >