< Luke 19 >

1 And having entered He was passing through Jericho.
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 And behold a man by name being called Zacchaeus and he himself was a chief tax collector and (he himself *N+kO) (was *k) rich;
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 And he was seeking to see Jesus who He is and not he was able because of the crowd, because in stature small he was.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 And having run (to the *no) front he went up into a sycamore-fig tree so that he may see Him, for (through *k) that [way] He was soon to pass.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 And as He came to the place, having looked up Jesus (he saw him and *K) said to him; Zacchaeus, having hurried do come down; today for in the house of you it behooves Me to stay.
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 And having hurried he came down and received Him rejoicing.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 And having seen [it] (all *N+kO) were grumbling saying that With a sinful man He has entered to stay.
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 Having stood then Zacchaeus said to the Lord; Behold the half my possessions Lord, to the poor I give; and if of anyone anything I have defrauded, I restore [it] fourfold.
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 Said then to him Jesus that Today salvation to the house this has come, because also he himself a son of Abraham is;
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 Came for the Son of Man to seek and to save that having been lost.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 When are hearing now they these things having proceeded He spoke a parable because near being to Jerusalem He and thinking they that immediately is about the kingdom of God to appear.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 He said therefore; A man certain of noble birth proceeded to a country distant to receive for himself a kingdom and to return.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 Having called then ten servants his own he gave to them ten minas and said to them; (Do trade *NK+o) (in that *NO) (until *k) I come back.
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 But the citizens of him were hating him and sent a delegation after him saying; Not we are willing [for] this [man] to reign over us.
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 And it came to pass on the returning of him having received the kingdom that he directed to be called to him servants these to whom (he had given *N+kO) the money, in order that he may know (who *k) what (they had gained by trading. *N+kO)
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 Came up then the first saying; lord, the mina of you ten (has produced *N+kO) more minas.
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 And He said to him; (well done *N+kO) good servant! Because in very little faithful you were, do be having authority you are over ten cities.
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 And came the second saying; The mina of you, lord, has made five minas.
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 He said then also to this one; And you yourself over do be five cities.
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 And another came saying; lord, behold the mina of you which I was keeping lying in a piece of cloth;
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 I was afraid for of you, because a man harsh you are; You take up what not you did lay down and you reap what not you did sow.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 He says (now *k) to him; Out of the mouth of you I will judge you, evil servant. You knew that I myself a man harsh am taking up what not I did lay down and reaping what not I did sow;
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 Then because of why not did you give my money to (the *k) bank, and I myself and I myself having come with interest maybe it collected
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 And to those having stood by he said; do take from him the mina and do give [it] to the [one] the ten minas having.
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 And they said to him; Master, he has ten minas.
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 I say (for *ko) to you that to everyone who is having will be given, from however the [one] not having even that which he has will be taken away (from of him. *ko)
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Furthermore the enemies of mine (these *N+kO) those not having been willing [for] me to reign over them do bring here and do slay them before me.
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 And having said these things He was going on ahead going up to Jerusalem.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 And it came to pass as He drew near to Bethphage and Bethany toward the mount which is being called Olivet He sent two of the disciples (of him *ko)
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 (speaking; *N+kO) do go into the ahead village, in which entering you will find a colt tied on which no [one] ever yet of men has sat; (and *no) having untied it do bring [it].
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 And if anyone you shall ask; Because of why do you untie [it]? thus will you say (to him: *k) Because the Lord of it need has.’
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 Having departed then those sent found [it] even as He had said to them.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 When are untying then they the colt said the masters of it to them; Why untie you the colt?
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 And they said: (that *no) The Lord of it need has.
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 And they led it to Jesus, and having cast (their *N+kO) garments on the colt they put on [it] Jesus.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 When is going then He they were spreading the garments (of them *NK+o) on the road.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 When is drawing near then he already at the descent of the Mount of Olives began all the multitude of the disciples rejoicing to praise God in a voice loud for (all *NK+o) which they had seen [the] mighty works
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 saying: Blessed [is] the coming King in [the] name of [the] Lord; In heaven peace, and glory in [the] highest.
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 And some of the Pharisees from the crowd said to Him; Teacher, do rebuke the disciples of You.
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 And answering He said (to them: *ko) I say to you (that *ko) if these (will be silent, *N+kO) the stones (will cry out. *N+kO)
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 And as He drew near, having seen the city He wept over (it *N+kO)
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 saying that If you had known (and indeed *k) in the day (of you *k) this even you yourself the [things] for peace (of you; *ko) Now however they are hidden from eyes of you.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For will come days upon you that (will cast around *N+kO) the enemies of you a barricade you and they will surround you and they will hem in you on every side
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 and will level to the ground you and the children of you within you and not will leave a stone upon (a stone *N+kO) within you, because which not you knew the season of visitation of you.
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 And having entered into the temple He began to cast out those selling (in to it *k) (and buying *K)
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 saying to them; It has been written: (And *no) (will be *N+kO) the house of Mine a house of prayer’; You yourselves however it made a den of robbers.’
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 And He was teaching every day in the temple; the however chief priests and the scribes were seeking Him to destroy and the foremost of the people,
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 And not they were finding what they may do; the people for all were hanging on His [words] listening.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luke 19 >