< John 13 >

1 Before now the feast of the Passover knowing Jesus that (came *N+kO) to him hour that He may depart out of world this to the Father, having loved [his] own who [were] in the world to [the] end He loved them.
Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
2 And supper (taking place, *N+kO) the devil already having put into the heart that he may betray Him (Judas *N+kO) [son] of Simon (Iscariot *NK+o)
Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
3 knowing (Jesus *K) that all things (has given *N+kO) to Him the Father into the hands, and that from God He came forth and to God He is going,
Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
4 He rises from the supper and lays aside the garments, And having taken a towel He girded Himself.
hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
5 After that He pours water into the basin and He began to wash the feet of the disciples and to wipe [them] with the towel with which He was having girded himself.
Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
6 He comes then to Simon Peter; (and *k) who says to Him (that [question]; *ko) Lord, You yourself my do wash feet?
Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
7 Answered Jesus and said to him; What I myself do you yourself not know presently, you will know however after these things.
Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
8 Says to Him Peter; certainly not shall You wash my feet to the age. Answered Jesus to him; only unless I shall wash you, not you have part with Me. (aiōn g165)
Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
9 Says to Him Simon Peter; Lord, not the feet of me only but also the hands and the head.
Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
10 Says to him Jesus; The [one] having bathed himself not has need (only *no) (except *N+KO) the feet to wash, but is clean wholly; and you yourselves clean are but not all.
Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
11 He knew for the [one who] was betraying Him; on account of this He said (that *no) Not all clean you are.
Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
12 When therefore He had washed the feet of them and taken the garments of Him and (he reclined *N+kO) again, He said to them; Do you know what I have done to you?
Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
13 You yourselves call Me: Teacher and Lord, and rightly you say; I am for.
Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
14 If therefore I myself washed your feet the Lord and the Teacher, also you yourselves ought of one another to wash the feet;
Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
15 A pattern for I gave you, that even as I myself did to you also you yourselves may do.
Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
16 Amen Amen I say to you; not is a servant greater than the master of him nor [is] a messenger greater than the [one who] having sent him.
Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
17 If these things you know, blessed are you if you shall do them.
Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
18 Not about all of you I speak; I myself know (whom *N+kO) I chose; but that the Scripture may be fulfilled: The [one] eating (with *k) (Me *N+kO) the bread lifted up against Me myself the heel of him.’
“Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
19 From now I am telling you before it comes to pass, so that (you may believe *NK+o) when it may happen that I myself am [He].
“Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
20 Amen Amen I say to you; the [one] receiving (maybe *N+kO) any I shall send, Me myself receives; the [one] now Me myself receiving, receives the [One] having sent Me.
Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
21 These things having said Jesus was troubled in spirit and He testified and said; Amen Amen I say to you that one of you will betray Me.
Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Were looking (therefore *KO) upon one another the disciples, being uncertain of whom He is speaking.
Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
23 There was (now *k) reclining one (of *no) the disciples of Him in the bosom of Jesus whom was loving Jesus;
Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
24 Motions therefore to him Simon Peter (and says to him *o) (to ask *NK+o) who maybe (it would be *NK+o) about whom He is speaking.
Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
25 (Having leaned then *N+kO) he (thus *NO) on the breast of Jesus he says to Him; Lord, who is it?
Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
26 Answers (therefore *O) Jesus; He it is to whom I myself (will dip *N+kO) the morsel (and *no) (will give *N+kO) (to him. *no) (And *k) (having dipped *N+kO) (then *NO) the morsel (He takes [it] and *NO) gives [it] to Judas [son] of Simon (Iscariot. *N+kO)
Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
27 And after the morsel, then entered into him Satan. Says therefore to him Jesus; What you enact, do enact quicker.
Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
28 This now no [one] knew of those reclining to what He spoke to him.
Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
29 Some for were thinking, since the money bag had Judas, for is saying to him Jesus; do buy what things need [of] we have for the feast, or to the poor that something he may give.
Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
30 Having received therefore the morsel he went out immediately; it was now night.
Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
31 When therefore he had gone out, says Jesus; Now has been glorified the Son of Man, and God has been glorified in Him,
Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32 If God is glorified in Him also God will glorify Him in (Him[self] *N+kO) and immediately will glorify Him.
Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
33 Little children, yet a little while with you I am. You will seek Me, and even as I said to the Jews that Where I myself go you yourselves not are able to come, also to you I say now.
“Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
34 A commandment new I give to you that you may love one another, even as I have loved you so also you yourselves may love one another.
“Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
35 By this will know all that to Me disciples you are, if love you shall have among one another.
Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
36 Says to Him Simon Peter; Lord, where go You? Answered to him Jesus; Where I go not you are able Me now to follow; you will follow however afterward (to me. *k)
Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
37 Says to Him Peter; Lord, because of why not am I able You (to follow *NK+o) presently? The life of mine for You I will lay down.
Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
38 (answers *N+kO) (to him *k) Jesus; The life of you for Me will you lay down? Amen Amen I say to you; certainly not [the] rooster (may crow *N+kO) until that (you will deny *N+kO) Me three times.
Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”

< John 13 >