< Jeremiah 46 >

1 Which it came [the] word of Yahweh to Jeremiah the prophet on the nations.
Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
2 Of Egypt on [the] army of Pharaoh Necho [the] king of Egypt which it was at [the] river of Euphrates at Carchemish which he struck down Nebuchadnezzar [the] king of Babylon in [the] year fourth of Jehoiakim [the] son of Josiah [the] king of Judah.
Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
3 Set in order shield and body shield and draw near for battle.
“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
4 Harness the horses and mount the warhorses and take your stand with helmets polish the spears put on the armor.
Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
5 Why? have I seen they [will be] terrified [they will be] turned back backwards and warriors their they will be crushed and flight they will flee and not they will turn back terror [will be] from round about [the] utterance of Yahweh.
Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
6 May not he flee the swift [one] and may not he escape the warrior north-ward on [the] side of [the] river of Euphrates they will stumble and they will fall.
Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
7 Who? [is] this [who] like the River he rises like rivers they surge waters his.
“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
8 Egypt like the River it rises and like rivers they surge waters and it has said I will rise I will cover [the] earth I will destroy a city and [the] inhabitants in it.
Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
9 Go up O horses and drive madly O chariotry so they may go forth the warriors Cush and Put [who] wield a shield and Ludites [who] wield [those who] bend a bow.
Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
10 And the day that [belongs] to [the] Lord Yahweh of hosts a day of vengeance to avenge himself from opponents his and it will devour [the] sword and it will be satisfied and it will take its fill from blood their for a sacrifice of [the] Lord Yahweh of hosts [will be] in [the] land of [the] north to [the] river of Euphrates.
Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
11 Go up Gilead and acquire balm O virgin of [the] daughter of Egypt for vanity (you have multiplied *QK) remedies [is] healing there not for you.
“Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
12 They will hear nations shame your and outcry your it will be full the earth for warrior over warrior they will stumble together they will fall both of them.
Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
13 The word which he spoke Yahweh to Jeremiah the prophet of [the] coming of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon to strike [the] land of Egypt.
Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
14 Declare in Egypt and make a proclamation in Migdol and make a proclamation in Memphis and in Tahpanhes say take your stand and prepare yourself for it will devour [the] sword around you.
“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
15 Why? will he be prostrated mighty [ones] your not he will stand for Yahweh he will push him.
Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
16 He will multiply [one who] stumbles also he will fall each to neighbor his and they said arise! - so let us return to people our and to [the] land of kindred our because of [the] sword of the oppressor.
Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
17 People will call out there Pharaoh [the] king of Egypt [is] a noise he has let pass by the appointed time.
Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
18 [by] [the] life Of me [the] utterance of the king [is] Yahweh of hosts name his that like Tabor among the mountains and like Carmel at the sea he will come.
“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
19 Baggage of exile make for yourself O inhabitant[s] [the] daughter of Egypt for Memphis a waste it will become and it will be made desolate from not inhabitant.
Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
20 [is] a heifer Beautifully beautiful Egypt a gadfly from [the] north [is] about to come [is] about to come.
“Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
21 Also hired soldiers its in midst its [are] like calves of [the] stall for also they they will turn they will flee together not they will stand their ground for [the] day of disaster their it will come on them [the] time of punishment their.
Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
22 Sound its [is] like snake [which] it goes for with an army they will come and with axes they will come to it like cutters of wood.
Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
23 They will cut down forest its [the] utterance of Yahweh that not it will be searched for they will be many more than locust[s] and not [belonged] to them number.
Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
24 It will be put to shame [the] daughter of Egypt it will be given in [the] hand of [the] people of [the] north.
Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
25 He says Yahweh of hosts [the] God of Israel here I [am] about to visit [judgment] to Amon from Thebes and on Pharaoh and on Egypt and on gods its and on kings its and on Pharaoh and on the [ones who] trust in him.
Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
26 And I will give them in [the] hand of [those who] seek life their and in [the] hand of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and in [the] hand of servants his and after thus it will settle like days of antiquity [the] utterance of Yahweh.
Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
27 And you may not you fear O servant my Jacob and may not you be dismayed O Israel for here I [am] about to save you from a distant [land] and offspring your from [the] land of captivity their and he will return Jacob and he will be undisturbed and he will be at ease and there not [will be one who] terrifies.
“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
28 You may not you fear O servant my Jacob [the] utterance of Yahweh that [am] with you I that I will make complete destruction on all the nations - where I have driven away you there towards and you not I will make complete destruction and I will discipline you to justice and certainly not I will leave unpunished you.
Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

< Jeremiah 46 >