< 2 Samuel 24 >

1 And again was the anger of Yahweh kindled against Israel, —so that he suffered David to be moved against them, saying, Go, count Israel and Judah.
Kisha hasira ya Yahwe ikawaka dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi kinyume chao kusema, “Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda.”
2 The king, therefore, said unto Joab, captain of the force, who was with him—Go to and fro, I pray thee, throughout all the tribes of Israel, from Dan even unto Beer -sheba, and number ye the people, —so shall I know the sum of the people.
Mfalme akamwambia Yoabu, jemedari wa jeshi, aliyekuwa pamoja naye, “Nenda upite katika kabila zote za Israeli, toka Dani mpaka Beersheba, uwahesabu watu wote, ili niweze kujua idadi kamili ya watu wanaofaa kwa vita.”
3 Then said Joab unto the king—Yea, Yahweh thy God add unto the people, how many soever they be, a hundredfold, and [suffer] the eyes of my lord the king, to see it, —but, my lord the king, wherefore doth he find pleasure in this thing?
Yoabu akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na aizidishe hesabu ya watu mara mia, na macho ya bwana wangu mfalme yaone ikifanyika. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme analitaka jambo hili?
4 Notwithstanding, the word of the king prevailed against Joab, and over the captains of the force, —so Joab went forth, with the captains of the force, before the king, to number the people—Israel.
Walakini neno la mfalme lilikuwa la mwisho dhidi ya Yoabu na dhidhi ya majemedari wa jeshi. Hivyo Yoabu na majemedari wakatoka mbele ya mfalme kuwahesabu watu wa Israeli.
5 And they passed over the Jordan, —and encamped in Aroer, on the right side of the city, that is in the midst of the ravine of Gad, even towards Jazer.
Wakavuka Yordani na kupiga kambi karibu na Aroeri, kusini mwa mji bondeni. Kisha wakasafiri kupitia Gadi mpaka Yazeri.
6 Thus came they to Gilead, and unto the land of Tahtim-hodshi, —and came to Dan-jaan, and round about Zidon;
Wakaja Gileadi na nchi ya Tahtimu Hodshi, kisha Dani, Jaani na karibu kuelekea Sidoni.
7 and entered the fortress of Tyre, and all the cities of the Hivites, and of the Canaanites, —and they went out to the South of Judah, even to Beer-sheba.
Wakafika ngome ya Tiro na miji yote ya Wahivi na Wakanaani. Kisha wakaenda Negebu katika Yuda huko Beersheba.
8 So, when they had gone to and fro throughout all the land, they came, at the end of nine months and twenty days, unto Jerusalem.
Walipokuwa wamepita katika nchi yote, wakarejea Yerusalemu mwishoni mwa miezi tisa na siku ishirini.
9 And Joab delivered up the sum of the number of the people, unto the king, —and there were found to be, in Israel, eight hundred thousand men of valour, drawing the sword, —and, the men of Judah, five hundred thousand men.
Ndipo Yoabu alipotoa taarifa ya hesabu kamili kwa mfalme kuhusu watu wawezao kupigana vita. Katika Israeli kulikuwa na watu 800, 000 jasiri wawezao kutoa upanga, na wale wa Yuda walikuwa watu 500, 000.
10 And the heart of David smote him, after he had reckoned up the people, —and David said unto Yahweh—I have sinned greatly, in what I have done, Now, therefore, O Yahweh, take away, I beseech thee, the iniquity of thy servant, for I have done very foolishly.
Ndipo moyo wa Daudi ukamchoma alipokuwa amewahesabu watu. Hivyo akamwambia Yahwe, “Kwa kufanya hivi nimetenda dhambi sana. Sasa, Yahwe, uiondoe hatia ya mtumishi wako, kwani nimetenda kwa upumbavu.”
11 And, when David arose in the morning, the word of Yahweh, had come unto Gad the prophet, the seer of David, saying:
Daudi alipoinuka asubuhi, neno la Yahwe likamjia nabii Gadi, mwonaji wa Daudi, kusema,
12 Go and speak unto David—Thus, saith Yahweh, Three things, do I offer thee, —choose thee one of them, that I may do it unto thee.
Nenda umwambie Daudi; 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: “Ninakupa mambo matatu. Uchague mojawapo.”
13 So Gad came in unto David, and told him, —and said to him: Shall there come unto thee seven years of famine in thy land? Or, for three months, wilt thou flee before thine enemies while, they, pursue thee? Or shall there be, for three days, pestilence in thy land? Now, consider and see, what, answer, I shall return to him that sent me.
Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je miaka mitatu ya njaa ije katika nchi yako? au miezi mitatu ukimbie kutoka kwa adui zako huku wakikufuatia? au kuwe na tauni ya siku tatu katika nchi yako? Amua sasa jibu gani nimrudishie aliyenituma.”
14 And David said unto Gad—I am in a great strait, —let us fall, I pray thee, into the hand of Yahweh, for, manifold, are, his compassions, but, into the hand of man, let me not fall.
Ndipo Daudi alipomwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa. Haya na tuanguke katika mikono ya Yahwe kuliko kuanguka katika mikono ya mwanadamu, kwani matendo yake ya rehema ni makuu sana.”
15 So Yahweh sent forth a pestilence throughout Israel, from the morning even unto the time appointed, —and there died of the people, from Dan even unto Beer-sheba, seventy thousand men.
Hivyo akatuma tauni juu ya Israeli kuanzia asubuhi kwa muda ulioamriwa, na watu sabini na tano elfu kutoka Dani mpaka Beersheba wakafa.
16 But, when the messenger stretched out his hand towards Jerusalem, to destroy it, then relented Yahweh as to the evil, and he said to the messenger who was destroying the people—Enough! now, stay thy hand. And, the messenger of Yahweh, was by the threshing-floor of Araunah the Jebusite.
Malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuuharibu, Yahwe akabadili nia yake kuhusu madhara, na akamwambia malaika aliyekuwa tiyari kuwaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako sasa.” Wakati huo malaika wa Yahwe alikuwa amesimama katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.
17 Then said David unto Yahweh, when he saw the messenger who was smiting the people, yea he said—Lo! I, have sinned, and, I, have done perversely, but what have, these sheep, done? Let thy hand, I pray thee, be against me, and against the house of my father!
Daudi alipomwona malaika aliyekuwa amewapiga watu, akamwambia Yahwe kusema, “Nimetenda dhambi, na nimetenda kwa upumbavu. Lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Tafadhari, mkono wako na uniadhibu mimi na familia ya baba yangu!”
18 And Gad came unto David, on that day, —and said unto him—Go up, rear thou unto Yahweh an altar, in the threshing-floor of Araunah the Jebusite.
Kisha Gadi akaja siku hiyo kwa Daudi na kumwambia, “Kwea na ujenge madhabahu kwa ajili ya Yahwe katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.”
19 So David went up, according to the word of Gad, as Yahweh had commanded.
Hivyo Daudi akakwea kama Gadi alivyomwelekeza kufanya, kama Yahwe alivyokuwa ameagiza.
20 And Araunah looked out, and saw the king, and his servants, passing over unto him—so Araunah went forth, and did homage unto the king, with his face to the ground.
Arauna akatazama na kumwona mfalme na watumishi wake wakikaribia. Ndipo Arauna akaondoka na kumsujudia mfalme uso wake mpaka juu ya ardhi.
21 Then said Araunah, Wherefore, hath my lord the king come unto his servant? And David said—To buy of thee the threshing-floor, to build an altar unto Yahweh, that the plague may be stayed from off the people.
Kisha Arauna akasema, “Kwa nini bwana wangu mfalme amekuja kwangu, mtumishi wake? Daudi akajibu, “Kununua uwanja wako wa kupuria, ili nimjengee Yahwe madhabahu, ili kwamba tauni iondolewe kwa watu.”
22 Then said Araunah unto David, Let my lord the king accept it and cause to ascend what is good in his own eyes, —see! the oxen for the ascending-sacrifice, and the threshing-sledges and ox-yokes for wood.
Arauna akamwambia Daudi, “Chukua liwe lako, bwana wangu mfalme. Ulifanyie lolote lolote lililojema machoni pako. Tazama, ng'ombe kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na miganda ya kupuria na nira kwa kuni.
23 The whole, did Araunah give, as a king to a king. And Araunah said unto the king, Yahweh thy God, accept thee!
Haya yote bwana wangu mfalme, mimi Arauna nakupa.” Kisha akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na awe nawe.”
24 But the king said unto Araunah—Nay! but I will, buy, it of thee, for a price, and will not cause to ascend unto Yahweh my God, offerings that have cost me nothing. So David bought the threshing-floor, and the oxen, for fifty shekels of silver;
Mfalme akamwambia Arauna, “Hapana, nahimiza kukinunua kwa thamani yake. Sitatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe chochote nisichokigharimia.” Hivyo Daudi akakinunua kiwanja cha kupuria na ng'ombe kwa shekeli hamsini za fedha.
25 and David built there an altar unto Yahweh, and caused to go up ascending-sacrifices and peace-offerings, —then was Yahweh entreated for the land, and the plague was stayed from Israel.
Daudi akajenga madhabahu kwa Yahwe pale na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Hivyo wakamsihi Yahwe kwa niaba ya nchi, hivyo akaizuia tauni katika katika Israeli yote.

< 2 Samuel 24 >