< Micah 6 >

1 Hear now what the Lord is saying: Arise, present your complaint before the mountains, let the hills hear your voice!
Sasa sikilizeni kile ambacho Yahwe asemacho, “Inuka na ueleze kesi yako mbele ya milima; acha milima isikie sauti yako.
2 Hear, mountains, the Lord’s accusation, listen, foundations of the earth. For the Lord has a case against his people. He has a dispute with Israel.
Sikilizeni madai ya Yahwe, enyi milima, na ninyi misingi mivumilivu ya dunia. Kwa kuwa Yahwe anavumilia pamoja na watu wake, na atapigana katika mahakama juu ya Israeli.”
3 “My people, what have I done to you. How have I displeased you? Answer me!
Watu wangu, nimefanya nini kwenu? nimewachosha mara ngapi? shuhudieni dhidi yangu!
4 For I brought you up from the land of Egypt, from the land of slavery I redeemed you. I sent Moses, Aaron, and Miriam to lead you.
Kwa kuwa niliwaleta kutoka nchi ya Msiri na kuwaokoa kutoka kwenye nyumba ya utumwa. Nawatuma Musa, Aruni, na Mariamu kwako.
5 My people, what did Balak, king of Moab counsel? And how did Balaam, the son of Beor, answer him? Remember now the journey from Shittim to Gilgal, so that you might realize the just deeds of the Lord.”
Watu wangu, kumbukeni ambavyo Balaki mfalme wa Moabu alivyotunga, na vile ambavyo Balamu mwana wa Beori alivyomjibu kama ulipokuwa ukienda kutoka kwa Gilgali, hivyo mnaweza kujua matendo ya haki ya Yahwe.”
6 With what should I come before the Lord? Bow myself before the God on high? Should I come before him with burnt-offerings, with calves a year old?
Je nilete nini kwa Yahwe, ninapoenda kumwinamia Mungu aliye juu? Je ninaweza kuja kwake na sadaka za kuteketeza, pamoja na ndama wenye mwaka mmoja?
7 Will the Lord be pleased with thousands of rams, With ten thousand streams of oil? Should I give him my firstborn son for my guilt, the fruit of my body for the sin of my soul?
Je Yahwe atapendezwa na maelfu ya kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe?
8 The Lord has told you what is good, what he demands of you: Only to do justice and love mercy, and to walk humbly with your God.
Amekwambia, mtu, kile kilicho bora, na kile ambacho Yahwe atakacho kutoka kwako: Kutenda haki, kupenda ukarimu, na kutembea kwa unyenyekevu pamoja na Mungu wako.
9 Listen! The Lord calls to the city! Listen, tribe and assembly of the city!
Sauti ya Yahwe inatangaza kwenye mji-hata sasa hekima hukukiri jina lako: “Kaa tayari kwa ajili ya fimbo, na kwa yule aliyeiweka.
10 “Can I forget the hoarded treasures in the houses of the wicked, and the accursed scant measure?
Kuna utajiri katika nyumba za waovu, na kipimo cha uongo hilo ni chukizo mno.
11 Can I leave her unpunished because of evil scales, and the bag of false weights?
Ningeweza kumfikira mtu kuwa hana hatia kama anatumia kipimo cha ulaghai, pamoja na mfuko wa kipimo wa udanganyifu?
12 Whose rich people are full of violence, her inhabitants liars, whose tongues speak deceit?
Matajiri wamejaa uharibifu, makazi yao yamesema uongo, na ulimi wao katika midomo yao unaudanganyifu.
13 “But I indeed, have begun to punish you, to lay you in ruins because of your sins.
Kwa hiyo nimekupiga kwa pigo linaloumiza, nimekufanya gofu kwa sababu ya dhambi zako.
14 You will eat but not be satisfied, your stomach empty within you. You will store up but lose everything, because whatever you save I will give to the sword.
Utakula lakini hutatosheka; utupu wako utabakia ndani yako. Utatunza mizigo mbali lakini hutahifadhi, na kile unachokihifadhi nitakitoa kwa upanga.
15 You will sow but not reap. You will tread the olives but have no oil for rubbing, tread grapes but drink no wine!
Utapanda lakini huatavuna; utazikusanya zaituni lakini hutajipaka mafuta; utasindika zabibu lakini hutakunywa divai.
16 “For you have followed the commands of Omri, and all the practices of the house of Ahab. You have acted in accord with their counsels, so I will give you up to ruin, the city’s inhabitants to derision. The nations will treat you with contempt!”
Kanuni zilizotengenezwa na Omri zimetunzwa, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu. Mnatembea kwa ushauri wao. Hivyo nitakufanya wewe, mji, gofu, na makazi yako jambo la zomeo, na matabeba dharau kama watu wangu.”

< Micah 6 >