< Ruth 2 >

1 Now Naomi was related through her husband to a very wealthy man of the family of Elimelech named Boaz.
Basi Elimeleki mme wa Naomi, alikuwa na jamaa aitwaye Boazi, aliye kuwa tajiri, na mtu maarufu.
2 Ruth the Moabite said to Naomi, ‘Let me now go into the fields and gather leftover grain behind anyone who will allow me.’ ‘Go, my daughter,’ she replied.
Ruth, Mmoabu, alimwambia Naomi, “Ngoja niende nikakusanye mabaki ya chakula katika shamba. Nitamfuata yeyote ambaye nitapata kibali machoni pake.” Hivyo naomi akamwambia, “Nenda, mwanangu.”
3 So she went to glean in the field after the reapers. As it happened, she was in that part of the field which belonged to Boaz, who was of the family of Elimelech.
Ruth alienda kuvuna kwenye shamba akiwafuata kwa nyuma wavunaji. Na kumbe ile sehemu ya shamba ilikuwa ni mali ya Boazi, aliyekuwa na mahusiano na Elimeleki.
4 When Boaz came from Bethlehem and said to the reapers, ‘The Lord be with you,’ they answered him, ‘May the Lord bless you.’
Tazama, Boazi alikuja kutoka bethelehemu na kuwaambia wavunaji, “Yahweh awe nanyi.” Wakamjibu, “Yahweh akubariki.”
5 ‘Whose girl is this?’ Boaz asked his servant who had charge of the reapers.
Ndipo Boazi akamwambia mtumishi wake aliyekuwa akiwasimamia wavunaji, “Vipi bwana huyu msichana ni wa nani?”
6 The servant who had charge of the reapers replied, ‘It is the Moabite girl who came back with Naomi from the territory of Moab.
Mtumishi msimamizi wa wavunaji alijibu na kusema, “Ni msichana Mmoabu aliyerudi na Naomi kutoka nchi ya Moabu.
7 She asked to be allowed to glean and gather sheaves after the reapers. So she came and has continued to work until now and she has not rested a moment in the field.’
Aliniambia, 'Tafadhali niruhusu kuvuna na kukusanya mabaki ya wavunaji.' Hivyo alikuja na ameendelea kuvuna toka asubuhi mpaka sasa, isipokuwa amepumzika kidogo katika nyumba.”
8 Then Boaz said to Ruth, ‘Listen, my daughter. Do not go to glean in another field nor leave this place, but stay here with my girls.
Kisha Boazi akamwambia Ruth, “Unanisikiliza, mwanangu? Usiende kuvuna kwenye shamba lingine; usiondoke shambani kwangu. Badala yake, baki hapa na wasichana wangu wa kazi.
9 Watch where the men are reaping and follow the gleaners. I have told the young men not to trouble you. When you are thirsty, go to the jars and drink of that which the young men have drawn.’
Yaelekeze tu macho yako kwenye shamba ambamo wanaume wanavuna na ufuatie nyuma ya wanawake wengine. Je, sikuwaelekeza wanaume wasikuguse? Na upatapo kiu, unaweza kwenda kunywa maji kwenye mtungi ambao wanaume wamejaza.”
10 Then she bowed low and said to him, ‘Why are you so kind to me, to take interest in me when I am just a foreigner?’
Ndipo akapiga magoti mbele ya Boazi, na kugusisha kichwa chake chini. Akamwambia, “Kwa nini nimepata kibali machoni pako, hata unijali mimi mgeni?”
11 Boaz replied, ‘I have heard what you have done for your mother-in-law since the death of your husband, and how you left your father and mother and your native land to come to a people that you did not know before.
Boazi akajibu na kumwabia, “Nimekwisha ambiwa, yote uliyo yafanya tangu mme wako afariki. Umewaacha baba yako, mama, na nchi uliyozaliwa kumfuata mama mkwe wako na kuja kwa watu usiowajua.
12 May the Lord repay you for what you have done, and may you be fully rewarded by the God of Israel, under whose wings you have come to take refuge.’
Yahweh akulipe kwa matendo yako. Yahweh akulipe kwa wingi, Mungu wa Israeli, ambaye chini ya mbawa zake umepata kimbilio.”
13 Then she said, ‘I trust I may please you, my lord, for you have comforted me and spoken kindly to your servant, although I am not really equal to one of your own servants.’
Ruth akasema, “Nipate kibali machoni pako, bwana wangu, kwa kuwa umenifariji, na umeongea wema kwangu, ingawa mimi sio mmoja wa watumishi wako wa kike.”
14 At mealtime Boaz said to Ruth, ‘Come here and eat some of the food and dip your piece of bread in the vinegar.’ So she sat beside the reapers, and he passed her some roasted grain. She ate until she was satisfied and had some left.
Wakati wa chakula Boazi alimwambia Ruth, “Njoo hapa, ule baadhi ya mikate, na uchovye kipande katika divai.” Alikaa kando ya wavunaji, na Boazi akampatia kiasi cha nafaka zilizo kaangwa. Ruth alikula mpaka alipotosheka na kusaza.
15 When she rose to glean, Boaz gave this order to his young men: ‘Let her glean even among the sheaves and do not disturb her.
Alipoinuka kwenda kuvuna, Boazi aliamuru vijana wake, akisema, “Mwacheni avune hata katika masuke, na msimwambie lolote baya.
16 Also pull out some for her from the bundles and leave for her to glean, and do not find fault with her.’
Na pia muachie baadhi ya masuke katika vifurushi kwa ajili yake, na muaache ili ayavune. Msimkemee.”
17 So she gleaned in the field until evening, then beat out what she had gleaned. It was about a bushel of barley.
Kwa hiyo alivuna mpaka jioni. Kisha akatenganisha nafaka na majani ambayo amevuna, nazo nafaka zilikuwa kama efa moja ya shairi.
18 Then she took it up and went into the town and showed her mother-in-law what she had gleaned. She also brought out and gave her that which she had left from her meal after she had had enough.
Akazibeba na kwenda katika mji. Ndipo mama mkwe wake aliona kile alichokivuna. Ruth pia alimletea mama mkwe wake nafaka zilizo kaangwa alizobakiza kwenye chakula chake.
19 ‘Where did you glean today, and where did you work?’ asked her mother-in-law. ‘A blessing on him who took notice of you!’ So she told her mother-in-law where she had worked. ‘The name of the man with whom I worked today,’ she said, ‘is Boaz.’
Mama mkwe wake akamwambia, “Umevunia wapi uliko vunia leo? Ulienda kufanyia wapi kazi? abarikiwe mtu aliye kusaidia.” Ndipo Ruth akamwambia mama mkwe wake kuhusu mtu aliye miliki shamba alilokuwa akifanya kazi. Alimwambia, “Jina la mtu ambaye alimiliki shamba nililokuwa nikifanya kazi ni Boazi.”
20 Naomi said to her daughter-in-law, ‘May the blessing of the Lord rest on this man who has not ceased to show his loving-kindness to the living and to the dead. The man,’ she added, ‘is a near relation of ours.’
Naomi akamwambia Ruth, “Abarikiwe na Yahweh, ambaye hakuondoa uaminifu wake kwa walio hai na wafu.” Naomi akamwambia, “Huyo mtu ni jamaa wa karibu nasi, ni jamaa yetu mkombozi.”
21 ‘He told me,’ Ruth said, ‘that I must keep near his young men until they have completed all his harvest.’
Ruth Mmoabu akamwambia, “Ni kweli, aliniambia, 'Ukae karibu na vijana wangu wa kiume mpaka watakapo maliza mavuno yangu yote.'”
22 Naomi said to Ruth, ‘It is best, my daughter, that you should go out with his girls because you might not be as safe in another field.’
Naomi akamwambia Ruth mke wa mtoto wake wa kiume, “Ni vizuri, mwanangu, kuwa uende pamoja na wasichana wake wa kazi, ili kwamba usije pata madhara yeyote katika shamba lolote.”
23 So she gleaned with the girls of Boaz until the end of the barley and wheat harvest; but she lived with her mother-in-law.
Kwa hiyo alikaa karibu na wafanyakazi wa kike ili avune mpaka mwisho wa mavuno ya shayiri na mavuno ya ngano. Na alikuwa akiishi pamoja na mama mkwe wake.

< Ruth 2 >