< Psalms 34 >

1 Of David, when he feigned madness in the presence of Abimelech, who drove him away, and he left. I will bless the Lord at all times, in my mouth will his praise be forever.
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 In the Lord will my heart make her boast, the humble will hear and be glad.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 O magnify the Lord with me and let us extol his name together.
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 I sought the Lord, and, in answer, he saved me from all my terrors.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 Look to him and you will be radiant, with faces unashamed.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 Here is one who was crushed, but cried and was heard by the Lord, and brought safe out of every trouble.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 The Lord’s angel encamps about those who fear him, and rescues them.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 O taste and see that the Lord is good, happy those who take refuge in him.
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Fear the Lord, all his people, for they who fear him lack nothing.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 Even young lions may be poor and hungry, but those who seek the Lord will not lack any good thing.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Come, children, listen to me. I will teach you the fear of the Lord.
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 Which of you is desirous of life, loves many and happy days?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Then guard your tongue from evil, and your lips from speaking deceit.
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Depart from evil, and do good; seek peace, and pursue it.
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 The eyes of the Lord are towards the righteous, his ears are towards their cry for help.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 The Lord sets his face against those who do evil, to root their memory out of the earth.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 When righteous cry, they are heard by the Lord, and he saves them from all their distresses.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 The Lord is near to the broken-hearted, he helps those whose spirit is crushed.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Many misfortunes befall the righteous, but the Lord delivers them out of them all.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 He guards all their bones, none are broken.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 Misfortune will slay the ungodly; those who hate the righteous are doomed.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 The Lord ransoms the life of his servants, and none will be doomed who takes refuge in him.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Psalms 34 >