< Psalms 3 >

1 A psalm of David, when he fled from his son Absalom. How many, Lord, are my foes! Those who rise up against me are many.
Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2 Many are those who say of me, ‘There is no help for him in his God.’ (Selah)
Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
3 But you, Lord, are shield about me, my glory, who lifts up my head.
Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4 When loudly I call to the Lord, from his holy hill he gives answer. (Selah)
Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5 I laid down and slept: now I wake, for the Lord sustains me.
Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6 I fear not the myriads of people who beset me on every side.
Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7 Arise, Lord: save me, my God, who strikes all my foes on the cheek, and shatters the teeth of the wicked.
Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
8 Victory belongs to the Lord: let your blessing descend on your people. (Selah)
Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

< Psalms 3 >