< Mark 3 >

1 And he entered again into the synagogue, and there was a man there who had his hand withered.
Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2 And They watched him, whether he would heal him on the Sabbath day, that they might accuse him.
Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3 And he said to the man with the withered hand, "Stand up in the middle."
Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, “Njoo hapa katikati.”
4 And he said to them, "Is it lawful on the Sabbath day to do good, or to do harm? To save a life, or to kill?" But they were silent.
Kisha, akawauliza, “Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao hawakusema neno.
5 And when he had looked around at them with anger, being grieved at the hardening of their hearts, he said to the man, "Stretch out your hand." He stretched it out, and his hand was restored.
Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, “Nyosha mkono wako!” Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6 And the Pharisees went out, and immediately conspired with the Herodians against him, how they might destroy him.
Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7 And Yeshua withdrew to the lake with his disciples, and a large crowd followed from Galil, and from Judea,
Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8 and from Jerusalem, and from Idumea, and beyond the Jordan, and those from around Tyre and Sidon. A large crowd, when they heard what great things he did, came to him.
Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9 And he told his disciples that a small boat should stay near him because of the crowd, so that they would not press on him.
Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10 For he had healed many, so that as many as had diseases pressed on him that they might touch him.
Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11 And the unclean spirits, whenever they saw him, fell down before him, and shouted, saying, "You are the Son of God."
Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!”
12 And he sternly warned them that they should not make him known.
Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13 And he went up into the mountain, and called to himself those whom he wanted, and they went to him.
Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14 And he appointed twelve, that they might be with him, and that he might send them out to preach,
naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15 to have authority to heal sicknesses and to cast out demons.
na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16 And he appointed the twelve. And to Shim'on he gave the name Peter;
Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17 and Jacob the son of Zavdai; and John the brother of Jacob (and he gave them the names Boanerges, which is to say, Sons of Thunder);
Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake “wanangurumo”),
18 and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and Jacob the son of Halfai, and Thaddaeus, and Shim'on the Zealot;
Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19 and Judah the Iskriot, who also betrayed him.
Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20 And he came into a house, and the crowd came together again, so that they could not so much as eat bread.
Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21 And when his family heard it, they went out to take charge of him: for they said, "He is out of his mind."
Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22 And the scribes who came down from Jerusalem said, "He has Beelzebul," and, "By the prince of the demons he casts out the demons."
Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, “Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo.”
23 And so he summoned them, and said to them in parables, "How can Satan cast out Satan?
Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24 And if a kingdom is divided against itself, that kingdom cannot stand.
Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25 And if a house is divided against itself, that house will not be able to stand.
Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26 And if Satan has risen up against himself, and is divided, he will not be able to stand, but has an end.
Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27 But no one can enter into the house of the strong man to plunder, unless he first binds the strong man; and then he will plunder his house.
“Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28 Truly I tell you, all human sins will be forgiven, including their blasphemies with which they may blaspheme;
“Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29 but whoever may blaspheme against the Ruach ha-Kodesh never has forgiveness, but is guilty of an everlasting sin"— (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 because they said, "He has an unclean spirit."
(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”)
31 And then his mother and his brothers came, and standing outside, they sent to him, calling him.
Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32 And a crowd was sitting around him, and they told him, "Look, your mother and your brothers are outside looking for you."
Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona.”
33 And he answered them, saying, "Who are my mother and my brothers?"
Yesu akawaambia, “Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?”
34 And looking around at those who sat around him, he said, "Look, my mother and my brothers.
Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, “Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 For whoever does the will of God, the same is my brother, and my sister, and mother."
Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu.”

< Mark 3 >