< Hebrews 1 >

1 God, having in the past spoken to the fathers through the prophets at many times and in various ways,
Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
2 in these last days has spoken to us by a Son, whom he appointed heir of all things, through whom also he made the ages. (aiōn g165)
lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
3 He is the radiance of his glory, the very image of his substance, and upholding all things by the word of his power, when he had made purification for sins, sat down on the right hand of the Majesty on high;
Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
4 having become so much better than the angels, as he has inherited a more excellent name than they have.
Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
5 For to which of the angels did he say at any time, "You are my Son. Today I have become your Father"? And again, "I will be his Father, and he will be my Son"?
Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
6 And again, when he brings in the firstborn into the world he says, "Let all the angels of God worship him."
Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
7 Of the angels he says, "Who makes his angels winds, and his servants a flame of fire."
Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
8 But of the Son he says, "Your throne, O God, is forever and ever, and the righteous scepter is the scepter of your Kingdom. (aiōn g165)
Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
9 You have loved righteousness, and hated iniquity; therefore God, your God, has anointed you with the oil of gladness above your companions."
Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
10 And, "In the beginning, Lord, you established the foundation of the earth. The heavens are the works of your hands.
Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 They will perish, but you remain; and they will all wear out like a garment.
Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
12 As a cloak, you will roll them up, and like a garment they will be changed. But you remain the same, and your years will have no end."
Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
13 But which of the angels has he told at any time, "Sit at my right hand, until I make your enemies the footstool of your feet?"
Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
14 Are they not all ministering spirits, sent out to do service for the sake of those who will inherit salvation?
Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.

< Hebrews 1 >