< Acts 3 >

1 Now Peter and John were going up into the temple at the hour of prayer, at three in the afternoon.
Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2 A certain man who was lame from his mother's womb was being carried, whom they put daily at the gate of the temple which is called Beautiful, to ask gifts for the needy of those who entered into the temple.
Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3 Seeing Peter and John about to go into the temple, he asked to receive gifts for the needy.
Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4 Peter, fastening his eyes on him, with John, said, "Look at us."
Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
5 He listened to them, expecting to receive something from them.
Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 But Peter said, "Silver and gold have I none, but what I have, that I give you. In the name of Yeshua the Messiah the Natzrati, get up and walk."
Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 He took him by the right hand, and raised him up. Immediately his feet and his ankle bones received strength.
Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8 Leaping up, he stood, and began to walk. He entered with them into the temple, walking, leaping, and praising God.
Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9 All the people saw him walking and praising God.
Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 They recognized him, that it was he who used to sit begging for gifts for the needy at the Beautiful Gate of the temple. They were filled with wonder and amazement at what had happened to him.
Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11 And as he held on to Peter and John, all the people ran together to them in the porch that is called Solomon's, greatly wondering.
Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12 When Peter saw it, he responded to the people, "You men of Israel, why are you amazed at this? Why do you fasten your eyes on us, as though by our own power or godliness we had made him walk?
Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13 The God of Abraham, Isaac, and Jacob, the God of our fathers, has glorified his Servant Yeshua, whom you delivered up, and denied in the presence of Pilate, when he had determined to release him.
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14 But you denied the Holy and Righteous One, and asked for a man who was a murderer to be granted to you,
Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15 and killed the Originator of life, whom God raised from the dead, to which we are witnesses.
Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16 By faith in his name, his name has made this man strong, whom you see and know. Yes, the faith which is through him has given him this perfect soundness in the presence of you all.
Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17 "Now, brothers, I know that you did this in ignorance, as did also your rulers.
“Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18 But the things which God announced by the mouth of all his prophets, that the Messiah should suffer, he thus fulfilled.
Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19 "Repent therefore, and turn again, that your sins may be blotted out, so that there may come times of refreshing from the presence of the Lord,
Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20 and that he may send the Messiah Yeshua, who was ordained for you before,
Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21 whom heaven must receive until the times of restoration of all things, which God spoke long ago by the mouth of his holy prophets. (aiōn g165)
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
22 For Moses indeed said to the fathers, 'The Lord your God will raise up a prophet for you from among your brothers, like me. You shall listen to him in all things whatever he says to you.
Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23 It will be, that every soul that will not listen to that prophet will be utterly destroyed from among the people.'
Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24 Yes, and all the prophets from Samuel and those who followed after, as many as have spoken, they also told of these days.
Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25 You are the children of the prophets, and of the covenant which God made with our fathers, saying to Abraham, 'And through your offspring all the families of the earth will be blessed.'
Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 God, having raised up his Servant, sent him to you first, to bless you, in turning away everyone of you from your wickedness."
Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”

< Acts 3 >