< 1 Peter 1 >

1 Peter, an emissary of Yeshua the Messiah, to the chosen ones who are living as foreigners in the Diaspora in Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia,
Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
2 according to the foreknowledge of God the Father, in sanctification of the Ruach, that you may obey Yeshua the Messiah and be sprinkled with his blood: Grace to you and peace be multiplied.
Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
3 Blessed be the God and Father of our Lord Yeshua the Messiah, who according to his great mercy caused us to be born again to a living hope through the resurrection of Yeshua the Messiah from the dead,
Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
4 to an incorruptible and undefiled inheritance that does not fade away, reserved in Heaven for you,
na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
5 who by the power of God are guarded through faith for a salvation ready to be revealed in the last time.
Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
6 Wherein you greatly rejoice, though now for a little while, if necessary, you have been grieved by various trials,
Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
7 that the genuineness of your faith, which is more precious than gold that perishes even though it is tested by fire, may be found to result in praise and glory and honor when Yeshua the Messiah is revealed—
Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
8 whom not having seen you love; in whom, though now you do not see him, yet believing, you rejoice greatly with joy inexpressible and full of glory—
Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
9 receiving the result of your faith, the salvation of your souls.
kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
10 Concerning this salvation, the prophets sought and searched diligently, who prophesied of the grace that would come to you,
Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
11 searching for who or what kind of time the Ruach of Messiah, which was in them, pointed to, when he predicted the sufferings of Messiah, and the glories that would follow them.
Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
12 To them it was revealed, that not to themselves, but to you, they ministered these things, which now have been announced to you through those who preached the Good News to you by the Ruach ha-Kodesh sent out from heaven; which things angels desire to look into.
Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
13 Therefore, prepare your minds for action, be sober and set your hope fully on the grace that will be brought to you when Yeshua the Messiah is revealed.
Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
14 As obedient children, do not be conformed to the desires as in your ignorance,
Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
15 but just as he who called you is holy, you yourselves also be holy in all of your behavior;
Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
16 because it is written, "You shall be holy; for I am holy."
Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
17 If you call on him as Father, who without respect of persons judges according to each man's work, pass the time of your living as foreigners here in reverent fear:
Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
18 knowing that you were redeemed, not with corruptible things, with silver or gold, from the useless way of life handed down from your fathers,
Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
19 but with precious blood, as of an unblemished and spotless lamb, namely the Messiah.
bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
20 He was chosen in advance before the foundation of the world, but was revealed in these last times for your sake,
Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
21 who through him are believers in God, who raised him from the dead, and gave him glory; so that your faith and hope might be in God.
Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22 Seeing you have purified your souls in your obedience to the truth in sincere brotherly affection, love one another from a pure heart fervently:
Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
23 having been born again, not of corruptible seed, but of incorruptible, through the living and abiding word of God. (aiōn g165)
Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
24 For, "All flesh is like grass, and all its glory like the flower in the grass. The grass withers, and its flower falls;
Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
25 but the word of the Lord endures forever." This is the word of Good News which was preached to you. (aiōn g165)
Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)

< 1 Peter 1 >