< 2 Samuel 24 >

1 Again the anger of Jehovah was kindled against Israel, and he moved David against them, saying, "Go, number Israel and Judah."
Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
2 The king said to Joab and the captains of the army, who were with him, "Now go back and forth through all the tribes of Israel, from Dan even to Beersheba, and number the people, that I may know the sum of the people."
Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
3 Joab said to the king, "Now may Jehovah your God add to the people, however many they may be, one hundred times; and may the eyes of my lord the king see it. But why does my lord the king delight in this thing?"
Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
4 Notwithstanding, the king's word prevailed against Joab, and against the captains of the army. Joab and the captains of the army went out from the presence of the king, to number the children of Israel.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
5 They crossed over the Jordan and began at Aroer, and from the city that is in the middle of the valley of Gad; then on to Jazer.
Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
6 Then they came to Gilead, and to the region of the Hethites, to Kedesh; and they came to Dan, and around to Sidon,
Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
7 and came to the stronghold of Tyre, and to all the cities of the Hivites, and of the Canaanites; and they went out to the south of Judah, at Beersheba.
Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
8 So when they had gone back and forth through all the land, they came to Jerusalem at the end of nine months and twenty days.
Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
9 Joab gave up the sum of the numbering of the people to the king: and there were in Israel eight hundred thousand valiant men who drew the sword; and the men of Judah were five hundred thousand men.
Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
10 David's heart struck him after that he had numbered the people. David said to Jehovah, "I have sinned greatly in that which I have done. But now, Jehovah, put away, I beg you, the iniquity of your servant; for I have done very foolishly."
Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
11 When David rose up in the morning, the word of Jehovah came to the prophet Gad, David's seer, saying,
Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
12 "Go and speak to David, 'Thus says Jehovah, "I offer you three things. Choose one of them, that I may do it to you."'"
“Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
13 So Gad came to David, and told him, and said to him, "Shall three years of famine come to you in your land? Or will you flee three months before your foes while they pursue you? Or shall there be three days' pestilence in your land? Now answer, and consider what answer I shall return to him who sent me."
Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
14 David said to Gad, "I am in distress. Let me fall now into the hand of Jehovah; for his mercies are great. Let me not fall into the hand of man."
Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
15 So Jehovah sent a pestilence on Israel from the morning even to the appointed time; and the destruction began among the people. And there died of the people from Dan even to Beersheba seventy thousand men.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
16 When the angel stretched out his hand toward Jerusalem to destroy it, Jehovah relented of the disaster, and said to the angel who destroyed the people, "It is enough. Now stay your hand." The angel of Jehovah was by the threshing floor of Araunah the Jebusite. And David lifted up his eyes and saw the angel of Jehovah standing between earth and the sky, having a drawn sword in his hand stretched out over Jerusalem. Then David and the elders, clothed in sackcloth, fell down on their faces.
Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
17 David spoke to Jehovah when he saw the angel who struck the people, and said, "Look, I have sinned, and I, the shepherd, have done great evil. But these sheep, what have they done? Please let your hand be against me, and against my father's house."
Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
18 Gad came that day to David, and said to him, "Go up, build an altar to Jehovah on the threshing floor of Araunah the Jebusite."
Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
19 David went up according to the saying of Gad, as Jehovah commanded.
Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
20 And Araunah looked out and saw the king and his servants coming on toward him, so Araunah went out and bowed himself before the king with his face to the ground.
Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
21 And Araunah said, "Why has my lord the king come to his servant?" David said, "To buy your threshing floor, to build an altar to Jehovah, that the plague may be stopped from afflicting the people."
Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
22 Araunah said to David, "Let my lord the king take and offer up what seems good to him. Look, the cattle for the burnt offering, and the threshing instruments and the yokes of the oxen for the wood."
Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
23 All these Araunah gave to the king." And Araunah said to the king, "May Jehovah your God accept you."
Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
24 The king said to Araunah, "No; but I will most certainly buy it from you for a price. I will not offer burnt offerings to Jehovah my God which cost me nothing." So David bought the threshing floor and the oxen for fifty shekels of silver.
Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
25 David built an altar to Jehovah there, and offered burnt offerings and peace offerings. So Jehovah responded to the plea for the land, and the plague was stayed from Israel.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.

< 2 Samuel 24 >