< Genesis 28 >

1 And Isaac called Jacob, and blessed him, and charged him, and said unto him, Thou shalt not take a wife from the daughters of Canaan.
Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
2 Arise, go to Padan-aram, to the house of Bethuel thy mother's father; and take thyself from there a wife of the daughters of Laban thy mother's brother.
Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
3 And God, the Almighty, bless thee, and make thee fruitful, and multiply thee, that thou mayest become a multitude of people;
Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
4 And may he give thee the blessing of Abraham, to thee, and to thy seed with thee; that thou mayest inherit the land of thy sojourn, which God gave unto Abraham.
Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
5 And Isaac sent away Jacob, and he went to Padan-aram, unto Laban, the son of Bethuel the Syrian, the brother of Rebekah, the mother of Jacob and Esau.
Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
6 And when Esau saw that Isaac had blessed Jacob, and sent him away to Padan-aram, to take himself from there a wife; and in blessing him had given him a charge, saying, Thou shalt not take a wife of the daughters of Canaan;
Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
7 And that Jacob had obeyed his father and his mother, and was gone to Padan-aram:
Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
8 Then saw Esau that the daughters of Canaan were evil in the eyes of Isaac his father;
Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
9 And Esau went unto Ishmael, and took Machalath the daughter of Ishmael, Abraham's son, the sister of Nebayoth in addition to his wives, to himself as wife.
Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
10 And Jacob went out from Beer-sheba, and went toward Charan.
Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
11 And he lighted upon a certain place, and tarried there all night, because the sun was set; and he took one of the stones of the place, and put it for his pillow, and laid himself down in that place.
Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
12 And he dreamed, and behold a ladder was set up on the earth, and the top of it reached to heaven; and behold, angels of God were ascending and descending on it.
Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
13 And, behold, the Lord stood above it, and said, I am the Lord, the God of Abraham thy father, and the God of Isaac: the land whereon thou liest, to thee will I give it, and to thy seed;
Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
14 And thy seed shall be as the dust of the earth, and thou shalt spread abroad to the west, and to the east, and to the north and to the south; and in thee and thy seed shall all the families of the earth be blessed.
Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
15 And, behold, I am with thee, and will keep thee whithersoever thou goest, and will bring thee again into this land; for I will not leave thee, until I have done what I have spoken to thee of.
Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
16 And Jacob awakened out of his sleep, and he said, Surely the Lord is present in this place; and I knew it not.
Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
17 And he was afraid, and said, How fearful is this place! this is none other but the house of God, and this is the gate of heaven.
Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
18 And Jacob rose up early in the morning, and took the stone that he had put for his pillow, and set it up for a pillar, and poured oil upon the top of it.
Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
19 And he called the name of that place Beth-el; but Luz was the name of that city in former times.
Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
20 And Jacob made a vow, saying, If God will be with me, and will keep me on this way which I am going, and will give me bread to eat, and raiment to put on,
Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
21 And I come again in peace to my father's house: then shall the Lord be my God;
hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
22 And this stone, which I have set for a pillar, shall be God's house; and of all that thou wilt give me I will surely give the tenth unto thee.
Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”

< Genesis 28 >