< Philemon 1 >

1 Paul, a prisoner of Jesus Christ, and Timothy [our] brother, unto Philemon our dearly beloved, and fellowlabourer,
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 And to [our] beloved Apphia, and Archippus our fellowsoldier, and to the church in thy house:
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Grace to you, and peace, from God our Father and the Lord Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 I thank my God, making mention of thee always in my prayers,
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 Hearing of thy love and faith, which thou hast toward the Lord Jesus, and toward all saints;
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 That the communication of thy faith may become effectual by the acknowledging of every good thing which is in you in Christ Jesus.
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 For we have great joy and consolation in thy love, because the bowels of the saints are refreshed by thee, brother.
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Wherefore, though I might be much bold in Christ to enjoin thee that which is convenient,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 Yet for love’s sake I rather beseech [thee], being such an one as Paul the aged, and now also a prisoner of Jesus Christ.
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 I beseech thee for my son Onesimus, whom I have begotten in my bonds:
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 Which in time past was to thee unprofitable, but now profitable to thee and to me:
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 Whom I have sent again: thou therefore receive him, that is, mine own bowels:
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 Whom I would have retained with me, that in thy stead he might have ministered unto me in the bonds of the gospel:
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 But without thy mind would I do nothing; that thy benefit should not be as it were of necessity, but willingly.
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 For perhaps he therefore departed for a season, that thou shouldest receive him for ever; (aiōnios g166)
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
16 Not now as a servant, but above a servant, a brother beloved, specially to me, but how much more unto thee, both in the flesh, and in the Lord?
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 If thou count me therefore a partner, receive him as myself.
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 If he hath wronged thee, or oweth [thee] ought, put that on mine account;
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 I Paul have written [it] with mine own hand, I will repay [it]: albeit I do not say to thee how thou owest unto me even thine own self besides.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Yea, brother, let me have joy of thee in the Lord: refresh my bowels in the Lord.
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 Having confidence in thy obedience I wrote unto thee, knowing that thou wilt also do more than I say.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 But withal prepare me also a lodging: for I trust that through your prayers I shall be given unto you.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 There salute thee Epaphras, my fellowprisoner in Christ Jesus;
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 Marcus, Aristarchus, Demas, Lucas, my fellowlabourers.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 The grace of our Lord Jesus Christ [be] with your spirit. Amen.
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< Philemon 1 >