< Genesis 36 >

1 Now these [are] the generations of Esau, who [is] Edom.
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
2 Esau took his wives of the daughters of Canaan; Adah the daughter of Elon the Hittite, and Aholibamah the daughter of Anah the daughter of Zibeon the Hivite;
Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
3 And Bashemath Ishmael’s daughter, sister of Nebajoth.
Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
4 And Adah bare to Esau Eliphaz; and Bashemath bare Reuel;
Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
5 And Aholibamah bare Jeush, and Jaalam, and Korah: these [are] the sons of Esau, which were born unto him in the land of Canaan.
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
6 And Esau took his wives, and his sons, and his daughters, and all the persons of his house, and his cattle, and all his beasts, and all his substance, which he had got in the land of Canaan; and went into the country from the face of his brother Jacob.
Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
7 For their riches were more than that they might dwell together; and the land wherein they were strangers could not bear them because of their cattle.
Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
8 Thus dwelt Esau in mount Seir: Esau [is] Edom.
Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
9 And these [are] the generations of Esau the father of the Edomites in mount Seir:
Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
10 These [are] the names of Esau’s sons; Eliphaz the son of Adah the wife of Esau, Reuel the son of Bashemath the wife of Esau.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
11 And the sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, and Gatam, and Kenaz.
Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
12 And Timna was concubine to Eliphaz Esau’s son; and she bare to Eliphaz Amalek: these [were] the sons of Adah Esau’s wife.
Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
13 And these [are] the sons of Reuel; Nahath, and Zerah, Shammah, and Mizzah: these were the sons of Bashemath Esau’s wife.
Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
14 And these were the sons of Aholibamah, the daughter of Anah the daughter of Zibeon, Esau’s wife: and she bare to Esau Jeush, and Jaalam, and Korah.
Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
15 These [were] dukes of the sons of Esau: the sons of Eliphaz the firstborn [son] of Esau; duke Teman, duke Omar, duke Zepho, duke Kenaz,
Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
16 Duke Korah, duke Gatam, [and] duke Amalek: these [are] the dukes [that came] of Eliphaz in the land of Edom; these [were] the sons of Adah.
Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
17 And these [are] the sons of Reuel Esau’s son; duke Nahath, duke Zerah, duke Shammah, duke Mizzah: these [are] the dukes [that came] of Reuel in the land of Edom; these [are] the sons of Bashemath Esau’s wife.
Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
18 And these [are] the sons of Aholibamah Esau’s wife; duke Jeush, duke Jaalam, duke Korah: these [were] the dukes [that came] of Aholibamah the daughter of Anah, Esau’s wife.
Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
19 These [are] the sons of Esau, who [is] Edom, and these [are] their dukes.
Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
20 These [are] the sons of Seir the Horite, who inhabited the land; Lotan, and Shobal, and Zibeon, and Anah,
Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
21 And Dishon, and Ezer, and Dishan: these [are] the dukes of the Horites, the children of Seir in the land of Edom.
Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
22 And the children of Lotan were Hori and Hemam; and Lotan’s sister [was] Timna.
Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
23 And the children of Shobal [were] these; Alvan, and Manahath, and Ebal, Shepho, and Onam.
Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
24 And these [are] the children of Zibeon; both Ajah, and Anah: this [was that] Anah that found the mules in the wilderness, as he fed the asses of Zibeon his father.
Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
25 And the children of Anah [were] these; Dishon, and Aholibamah the daughter of Anah.
Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
26 And these [are] the children of Dishon; Hemdan, and Eshban, and Ithran, and Cheran.
Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
27 The children of Ezer [are] these; Bilhan, and Zaavan, and Akan.
Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
28 The children of Dishan [are] these; Uz, and Aran.
Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
29 These [are] the dukes [that came] of the Horites; duke Lotan, duke Shobal, duke Zibeon, duke Anah,
Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
30 Duke Dishon, duke Ezer, duke Dishan: these [are] the dukes [that came] of Hori, among their dukes in the land of Seir.
Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
31 And these [are] the kings that reigned in the land of Edom, before there reigned any king over the children of Israel.
Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
32 And Bela the son of Beor reigned in Edom: and the name of his city [was] Dinhabah.
Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
33 And Bela died, and Jobab the son of Zerah of Bozrah reigned in his stead.
Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
34 And Jobab died, and Husham of the land of Temani reigned in his stead.
Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
35 And Husham died, and Hadad the son of Bedad, who smote Midian in the field of Moab, reigned in his stead: and the name of his city [was] Avith.
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
36 And Hadad died, and Samlah of Masrekah reigned in his stead.
Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
37 And Samlah died, and Saul of Rehoboth [by] the river reigned in his stead.
Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
38 And Saul died, and Baal-hanan the son of Achbor reigned in his stead.
Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
39 And Baal-hanan the son of Achbor died, and Hadar reigned in his stead: and the name of his city [was] Pau; and his wife’s name [was] Mehetabel, the daughter of Matred, the daughter of Mezahab.
Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
40 And these [are] the names of the dukes [that came] of Esau, according to their families, after their places, by their names; duke Timnah, duke Alvah, duke Jetheth,
Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
41 Duke Aholibamah, duke Elah, duke Pinon,
Oholibama, Ela, Pinoni,
42 Duke Kenaz, duke Teman, duke Mibzar,
Kenazi, Temani, Mbza,
43 Duke Magdiel, duke Iram: these [be] the dukes of Edom, according to their habitations in the land of their possession: he [is] Esau the father of the Edomites.
Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.

< Genesis 36 >